• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

NEWALA DC YAADHIMISHA SIKU YA LISHE KITAIFA KWA VITENDO

Posted on: October 31st, 2024

NEWALA, MTWARA

Halmashauri ya wilaya ya Newala Jana Oktoba 30,2024 imeadhimisha siku ya Lishe kitaifa katika Kijiji cha Makukwe ikiwa na  kauli mbiu isemayo "Mchongo ni Afya yako, zingatia unachokula"

  Maadhimisho hayo yamefanyika yakiwa na lengo la kutoa elimu ya Lishe kwa jamii kwa kuzingatia mapendekezo ya mwongozo wa kitaifa wa chakula na ulaji unaofaa kwa Afya Bora

Aidha  wataalam wa Afya na Lishe wametoa  elimu ya nadharia ikiwemo maana ya Lishe Bora,umuhimu wa chanjo na jiko darasa kwa vitendo ambapo Jamii imejifunza  mapishi ya uji ulioboreshwa wenye makundi 6 ya vyakula muhimu kwa ajili ya kukua vyema, kujenga mwili lakini pia kuimarisha Kinga ya mwili.

Akitoa elimu, Afisa lisha wilaya Bi Christina Lukinisha amesema ili lishe iwe Bora ni muhimu iwe na mchanganyiko wa vyakula mbalimbali kama vile protini kutoka kwenye nyama na Jamii ya kunde ,vyakula vya wanga, mbogamboga, mafuta, madini , matunda na maji kwa wingi.

Amesema licha ya watu wengi kujua umuhimu wa Lishe Bora lakini imekuwa tofauti kwa baadhi ya familia nyingi kwani kumekuwa na tabia ya kula chakula cha aina moja ambapo inasababisha watu kuwa na hali duni kiafya ambayo ndio chanzo cha magonjwa mbalimbali hatari.

" Nitoe rai kwa wananchi kujenga utamaduni wa kula Lishe Bora yenye mchanganyiko wa vyakula mbalimbali kwani inasaidia kupunguza vifo vya watoto vinavyotokana na Lishe duni" Amesema Lukinisha


Aidha huduma za Afya zilizotolewa kwa  katika maadhimisho ni Pamoja naTathmini ya Hali ya lishe na upimaji wa hali ya lishe na magonjwa yasiyoambukizwa,Elimu ya ulaji unaofaa kutoka makundi sita ya chakula,Jiko darasa,huduma za afya ikiwemo umuhimu wa chanjo na kumaliza chanjo,huduma za ustawi wa jamii,umuhimu wa wajawazito kuwahi kliniki, upimaji wa saratani ya shingo ya uzazi na uchangiaji wa damu.

Wataalam wa Afya walioshiriki katika utoaji wa huduma za afya na Elimu ni Christine Rukinisha- Afisa Lishe wa Wilaya,Jane Mgaza - Afisa Lishe, Stelina Ndokole- Afisa Chanjo,Jamila Nalinga - katibu wa afya na Saidi Mwengele Afisa Afya

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa