Mkuu wa Wilaya ya Newala, Mheshimiwa Alhaji Rajabu Kundya, amekabidhi unga wa sembe, sabuni na bidhaa nyingine za matumizi ya kila siku kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Ndugu Duncan Thebas, kwa ajili ya wanafunzi wa Kitengo cha Elimu Maalumu katika Shule ya Msingi Kitangari. Tukio hilo lilifanyika Februari 10, 2026 na ni sehemu ya mchango wa wachukuzi wa korosho wanaoendelea kuunga mkono jitihada za kusaidia makundi maalumu katika jamii.
Akizungumza wakati wa makabidhiano, Mheshimiwa Kundya alisisitiza umuhimu wa kuwajali watoto wenye mahitaji maalumu na kuhakikisha wanapata elimu bora katika mazingira rafiki. Pia aliagiza Halmashauri kuboresha miundombinu na huduma zinazowawezesha watoto hao kujifunza kwa ufanisi.
Baada ya kupokea msaada huo, Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Duncan Thebas alikabidhi kwa walimu wa shule hiyo kwa niaba ya wanafunzi. Walimu walitoa shukrani kwa Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya na wachangiaji wote kwa msaada uliotolewa, wakisema utaboresha mazingira ya ujifunzaji na ustawi wa wanafunzi wenye mahitaji maalumu.
@tamisemi
@mtwarars_habari
@msemajimkuuwaserikali
@dc_newala
@newalafmtz
Kitangari,Newala
Anuani ya Posta: P.O. Box 16
Simu: +255232410251
Mobile:
Barua pepe: ded@newaladc.go.tz
Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa