Marafiki wa Landsberg kutoka Ujerumani wamekabidhi vitendea kazi vya mifumo ya solar kwa Halmashauri ya Wilaya ya Newala kama sehemu ya kuimarisha miradi ya maendeleo katika sekta za afya na elimu. Makabidhiano hayo yalifanyika Februari 10, 2026 katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) kilichojadili na kupitia Rasimu ya bajeti ya Mwaka wa Fedha 2026/2027, yenye makadirio ya Shilingi bilioni 25.7 ambazo zimepangwa kutekeleza miradi ya maendeleo na kuboresha huduma za kijamii.
Vifaa hivyo vilikabidhiwa kwa niaba ya Wafadhiri wa Wananchi wa Ujerumani na Mratibu wa Landsberg Tanzania, Ndugu Sigfried Jordan Hittu na kuwakabidhi Viongozi wa Newala akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Newala, Mheshimiwa Mwangi Rajabu Kundya, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Ndugu Duncan Thebas.
Aidha, viongozi hao walivikabidhi kwa mafundi wa mifumo ya solar watakaosimamia matengenezo katika maeneo yenye miradi ya afya na elimu inayotumia Nishati ya Solar inayofadhiliwa na Marafiki wa Landsberg. Viongozi hao waliishukuru Landsberg na wananchi wa Ujerumani kwa msaada huo, wakisema umeimarisha zaidi mahusiano na ushirikiano baina ya Landsberg na Halmashauri ya Wilaya ya Newala katika kuboresha huduma kwa wananchi.
@tamisemi
@msemajimkuuwaserikali
@mtwarars_habari
@dc_newala
@landkreis.landsberg
Kitangari,Newala
Anuani ya Posta: P.O. Box 16
Simu: +255232410251
Mobile:
Barua pepe: ded@newaladc.go.tz
Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa