• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Wazazi waaswa kuutambua umuhimu wa elimu.

Posted on: July 11th, 2018

Wazazi wote Wilayani Newala, wameaswa kuutambua umuhimu wa Elimu kwa watoto wao ukizingatia kuwa maisha ya sasa yanahitaji taifa lililo elimika zaidi kwa msingi wa maisha.

Wito huo umetolewa na kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bwana Alford Mpanda katika sherehe za maadhimisho ya juma la Elimu kiwilaya, yaliyofanyika jana tarehe 10/07/2018 katika shule ya msingi Kitangali Mazoezi Wilayani Newala.

Bwana Mpanda amesema kuwa, wazazi wana jukumu kubwa la kufualitila maendeleo ya watoto wao shuleni ili waweze kufanya vizuri, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanakuwa na tabia njema na nidhamu wakati wote, jambo litakalopelekea kuwasaidia walimu katika kuwafundisha na kuwalea vizuri wakati wote wa masomo yao.

Aidha wadau wote wa elimu pamoja na wazazi kwa ujumla wametakiwa kuhakikisha wanawafatilia pia watoto wenye mahitaji maalumu, ili nao waweze kupata haki yao ya msingi katika elimu, kwani kumekuwa na kawaida kwa baadhi ya wazazi kuwatenga na kuwaficha watoto walemavu, jambo linalopelekea kuwakosesha elimu na kujifunza mambo mbalimbali.

Kwa upande wa kitengo cha elimu maalum katika shule ya Kitangali Mazoezi, mkuu wa kitengo hicho Mwalimu Jafari Mnambe, amesema kazi kubwa wanayoifanya kwa sasa, ni kuwabaini watoto  wenye mahitaji maalum katika vijiji vyote vya Tarafa ya Kitangali, kuwasajili shule na kuwabadilisha tabia zao za nyumbani, ili wajifunze maisha ya shule ambayo ni ya kimtaala wa elimu ya msingi.

Pamoja na changamoto za umbali na nyinginezo zikiwemo kukosekana kwa usafiri wa kutembelea shule mbalimbali, kitengo hicho cha elimu maalum, kiliweza kutembelea shule za kata nne za Maputi, Kitangali, Vihokoli na Nandwahi, ambapo katika ziara hiyo walifanikiwa kuwabaini watoto wenye mahitaji maalum ili wajiunge na wenzao waliopo katika kitengo cha elimu maalum kilichopo shule ya msingi Kitangali Mazoezi.

Baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi na sekondari za Tarafa ya Kitangali wakionyesha mabango yenye ujumbe mbalimbali wa elimu wakati wa maandamano ya kilele cha maadhimisho ya juma la elimu, yaliyofanyika tarehe 10/07/2018 katika shule ya msingi Kitangali Mazoezi.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya juma la elimu kwa mwaka huu wa 2018 ni “Stadi za KKK ni msingi wa elimu, tuwekeze katika elimu kwa uchumi wa viwanda”

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa