• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

MAFUNZO YA UANDAJI WA MIPANGO NA BAJETI KWA MAAFISA BAJETI

Posted on: October 11th, 2025

MAAFISA bajeti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala wametakiwa kuhakikisha mipango na bajeti wanazoandaa zinaendana na mahitaji halisi ya wananchi, zinakuwa shirikishi, zinatekelezeka na zinazingatia uwazi pamoja na uwajibikaji katika hatua zote za maandalizi.


Wito huo umetolewa jana na Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Ndugu Sylvester Ngonyani, wakati akifungua mafunzo ya Uandaji wa Mipango na Bajeti kwa Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.


Mafunzo hayo ni maandalizi ya bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027, ambapo utaratibu huu hufanyika kila mwaka kwa lengo la kuongeza ufanisi katika maandalizi na utekelezaji wa bajeti zinazogusa mahitaji ya wananchi. Ngonyani alisisitiza umuhimu wa kushirikisha ngazi zote katika michakato ya upangaji bajeti ili kuhakikisha mipango inayoandaliwa inatekelezeka kwa uhalisia.


Kwa upande wake, Afisa Bajeti (Mwezeshaji )wa mafunzo hayo kutoka Idara ya Mipango, Ndugu Aza  Macha, aliwasilisha mada kuhusu Uandaji wa Mipango na Bajeti katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, akisisitiza umuhimu wa kuwa na mipango yenye sifa za SMART—yaani mahsusi, inapimika, halisi, yenye muda maalum na inayotekelezeka.


Aidha, Ndugu Andrew Nyumayo, SN. DHRO, ambaye ni miongoni mwa washiriki wa mafunzo hayo, alielezea kufurahishwa na mafunzo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi kikamilifu. “Tumejifunza mambo muhimu sana, nitahakikisha tunazingatia ushirikishwaji wa watumishi wote katika kila idara na kitengo wakati wa maandalizi ya bajeti,” alisema Nyumayo.


Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya TAMISEMI yaliyopo kwenye Muongozo wa Uandaji wa Mipango na Bajeti, yakiwa na lengo la kuimarisha utendaji wa Serikali za Mitaa katika kusimamia rasilimali za umma kwa tija na maendeleo endelevu ya wananchi.

@ortamisemi

@mtwarars_habari

@msemajimkuuwaserikali

@newalafmtz

@chikaladigitaltv

@kizurdigital

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA UANDAJI WA MIPANGO NA BAJETI KWA MAAFISA BAJETI

    October 11, 2025
  • NEWALA DC YAENDELEA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU

    October 09, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA

    October 02, 2025
  • FURSA ZA MIKOPO NEWALA DC

    September 11, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa