• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Wakazi wa Newala watakiwa kupenda elimu, kuchapa kazi na kujiletea maendeleo binafsi

Posted on: January 30th, 2020

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Gasper Byakanwa alipofanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Newala siku ya Jumatano tarehe 29/01/2020.

Katika ziara hiyo Mhe. Byakanwa amekemea wazazi wasiowapeleka watoto shule na kuagiza watoto wote wanaotakiwa kuripoti shuleni waripoti haraka. Akisisitiza jambo hilo, Mhe. Byakanwa katika kijiji cha Nanda, kata ya Muungano, Halmashauri ya Wilaya ya Newala wazazi waliobainika kutokuwapeleka watoto shule walikamatwa na kupelekwa mahakamani ili kulipa faini kwa kutotekeleza wajibu wao wa kuwapeleka watoto shule.

Akiendelea na ziara hiyo, Mhe. Byakanwa pia amewaagiza Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata wote kuhakikisha vijana wanaoishi katika maeneo yao ya utawala wanafanya kazi na si kukaa vijiweni.

"Vijana wengi hawafanyi kazi, wanakaa vijiweni,  kucheza pool table, kula na kulala wakiwategemea wazazi kuwafanyia kazi. Kuanzia leo nataka kila kijana aonyeshe shamba lake na shughuli anayofanya na kuna timu maalum itakuja kuhakiki " alisema Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Byakanwa.

Ziara hiyo pia ilihusisha kusuluhisha migogoro ya mipaka kati ya maeneo ya shule na mashamba ya wanakijiji ambapo Mhe. Byakanwa ameagiza mipaka yote ya shule kuainishwa na wanakijiji kutovamia maeneo ya shule kwa shughuli zozote zikiwemo za kilimo.

"Mkoa ninaouongoza mimi, ninataka uwe ni wa watu wanaopenda elimu, wachapa kazi na wanaojiletea maendeleo yao wenyewe", alisema Mhe. Byakanwa.
Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Byakanwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Newala ni ya kikazi na ilihusisha kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa, vyoo vya wanafunzi na walimu, mahudhurio ya wanafunzi shuleni na kuzungumza na wananchi ambapo shule za sekondari Makukwe na Mpotola, na shule za msingi Nanda na Mtunguru B zilitembelewa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa