• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Viongozi wasiofaa waondolewa vyama vya msingi

Posted on: July 26th, 2018

Serikali imewaondoa viongozi wasiofaa wa vyama vya msingi vya Newala na Tandahimba katika utendaji wao kufuatia ubadhilifu na kukosa sifa za utendaji katika vyama vya msingi.

Hatua hiyo imefikia mara baada ya uchunguzi uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa na kamati yake ya ulinzi na usalama kwa Wilaya zote mbili za Newala na Tandahimba, na kubainisha rasmi katika mkutano maalum uliofanyika jana tarehe 25/07/2018 katika ghala la TANECU, uliohusha chama cha ushirika TANECU pamoja na viongozi wa vyama vyote vya msingi wa Newala na Tandahima.

Mhe. Byakanwa alisema kwa upande wa Tandahimba, wamewaondoa viongozi takriban 72 waliohusika na upotevu wa pesa za wakulima katika msimu wa mwaka 2017/2018 na kwamba chama kilichoongoza zaidi kwa upotevu wa pesa ni kile kilichopoteza milioni 176 mbali na vyama vingine ambavyo vimehusika kupoteza viwango tofauti tofauti, na kwa upande wa Newala viongozi 12 walioondolewa ni kutokana na kuwa na elimu ya darasa la saba kwa mujibu wa sheria, na viongozi sita nao wamehusika katika ubadhilifu.

Aidha viongozi wote waliohusika kwenye ubadhilifu na waliokosa elimu ya kidato cha nne lakini bado wapo kwenye ushirika wataondolewa, wenye elimu ya darasa la saba watakaobakia ni wale waliochaguliwa tu, na kwa watendaji wa kuajiriwa ni lazima wawe na elimu ya kuanzia kidato cha nne, lengo ni kuusafisha ushirika na kuufanya ushirika uwe na watu wanaojua majukumu yao na wanaoweza kusimamia maslahi ya wanachama wao na sio wale wanaoingia kwenye ushirika kwa malengo ya kujinufaisha wenyewe.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara amewataka wakulima wote wa Newala na Tandahimba kuhakikisha wanafungua akaunti zao binafsi kabla ya msimu wakorosho wa 2018/2019 kuanza, kwani jambo lililochangia kuchelewesha malipo ya wakulima katika msimu uliopita ni kutokana na wakulima wengi kukosa akaunti zao wenyewe na kuchelewa kufungua akaunti, hivyo kila mkulima ni lazima awe na akaunti yake kabla ya msimu kuanza na ambae hatakuwa na akaunti yake hatapata malipo.

Kufuatia hilo Mhe. Byakanwa amewaagiza makatibu na watendaji wote wa AMCOS kuhakikisha kabla ya msimu huu kuanza wanaorodhesha na kubandika majina ya wakulima wao au wataokauza korosho kwao, akaunti namba zao na benki zao ili uwe muongozo wa kuwatambua na kurahisisha mchakato wa malipo yao, na maafisa ushirika wasimamie hilo.

Msimu wa korosho wa mwaka 2018/2019 unatarajiwa kuwa na utofauti mkubwa utakaorahisisha mchakato wa malipo na kuleta tija kwa wakulima.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa