Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kung'ara kwa uongozi wake thabiti unaojikita katika kuimarisha huduma za afya kwa Watanzania wote. Kupitia Ilani ya CCM, Serikali ya Awamu ya Sita imefanya kazi kubwa ya kuongeza vituo vya afya kutoka 6,081 hadi 7,713 kufikia Aprili 2025, ikiwa ni ongezeko la asilimia 26.80. Hili ni jambo la kujivunia kwani linaonesha dhamira ya kweli ya kuwahudumia wananchi.
Kwa uongozi wake mahiri, Mhe. Rais Samia ameihakikishia Tanzania huduma bora za afya kwa kuwekeza katika ujenzi na ukarabati wa Zahanati 1,158, Vituo vya Afya 345, na Hospitali za Halmashauri 129. Hili limeleta mapinduzi makubwa ya upatikanaji wa huduma za afya karibu na wananchi, hasa maeneo ya vijijini ambayo awali yalikuwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya afya.
Uwekezaji huu si wa majengo pekee, bali unakwenda sambamba na utoaji wa vifaa tiba, ajira kwa watumishi wa afya, pamoja na kuimarisha huduma rafiki kwa mama na mtoto. Rais Samia amekuwa kinara wa kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya afya kwa kuwathamini watumishi wa sekta hii muhimu na kuweka kipaumbele ustawi wa jamii.
Kupitia dira yake ya upendo, mshikamano na maendeleo jumuishi, Rais Samia ameweka misingi imara ya afya kwa wote. Matokeo ya kazi yake yanaonekana wazi na kuthibitisha kuwa Tanzania iko katika mwelekeo sahihi wa kufikia huduma bora za afya kwa kila Mtanzania. Hakika, huu ni ushahidi wa kiongozi mwenye maono, huruma, na ujasiri wa kuleta mabadiliko ya kweli.
# UTEKEZAJI WA ILANI YA CCM UNAONEKANA KWA ASILIMIA
Kitangari,Newala
Anuani ya Posta: P.O. Box 16
Simu: +255232410251
Mobile:
Barua pepe: ded@newaladc.go.tz
Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa