• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

RC MTWARA AFANYA ZIARA YA KUJITAMBULISHA WILAYA YA NEWALA

Posted on: January 19th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bw. Galasius Gasper Byakanwa amefanya ziara ya siku mbili kuanzia tarehe 18 mpaka 19 mwezi Januari 2018 katika Wilaya ya Newala kwa lengo la kujitambulisha kwa wananchi anaowaongoza.

Bw. Galasius Byakanwa akizungumza na watumishi wa wilaya ya Newala katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Newala

Katika ziara yake, alizungumza na watumishi wa Newala, alishiriki kupanda miche ya korosho, kukagua ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Mji Newala na kuzindua ugawaji wa pikipiki na guta kwa vikundi kupitia TAMOSA.

Akizungumza na wananchi wa Newala, Bw. Byakanwa amewataka kudumisha amani na utulivu miongoni mwao kwa kuwa ndiyo chimbuko kuu la maendeleo. Pia amewataka wananchi wa Newala kurudi kwenye misingi ya utanzania kwa kutambua wenyeji na wageni kwa kuanzisha daftari la makazi ambalo litasaidia kujua wakazi wa eneo husika kwa majina, maeneo wanayoishi na shughuli wanazofanya.

Bw. Byakanwa amesisitiza juu ya zoezi linaloendelea la uandikishaji na utoaji wa vitambulisho vya taifa, ambapo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo ili wapate vitambulisho hivyo kwa kuwa vitawasaidia katika mambo mbalimnbali yakiwemo kumtambulisha mtu kuwa ni mtanzania, kutumika kuomba pasi ya kusafiria ‘passport’ na kufungulia akaunti.

Pia amesisitiza kuzingatia mipangomiji kwa maafisa ardhi kuhakikisha wanatoa vibali vya ujenzi kabla ya zoezi la ujenzi kuanza na kupima maeneo na kuyatenga kwa kuzingatia matumizi bora ya ardhi.

Akiendelea kuzungumza, Bw. Byakanwa amewataka wananchi wa Newala kujiunga na mfuko wa afya ya jamii (CHF) kwa kuagiza walengwa wa kaya masikini wanaosaidiwa na Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) kujiunga na CHF kwa kuchangia shilingi elfu kumi kwa kila kaya na wakatwe fedha hizo katika malipo yao.

Pia amewatoa hofu wakazi wa Newala juu ya swala la ukatikaji wa mara kwa mara wa umeme kwa kuwaeleza kuwa hali hiyo inasababishwa na uwezo mdogo wa uzalishaji wa umeme kwa mashine tulizonazo ambao ni megawatts 15.8 na kwa sasa utaratibu wa kuunganishwa kwenye gridi ya taifa unafanyika na pia zimeagizwa mashine mbili zitakazosaidia kuongeza uzalishaji wa umeme hadi kufikia megawatts 22.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bw. Byekanwa akizindua moja ya pikipiki ya vikundi vya vijana

Bw. Bakanwa pia ametumia ziara hiyo kukataza walimu kuchangisha michango kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari na kuwataka walimu kuusoma vizuri waraka wa elimu bure kwa kuwa ndio unaotuongoza kuzuia michango hiyo.

Pia ziara hiyo ilihusisha utembelewaji wa shamba la NEDECO lililopo katika kijiji cha Nanguruwe wilaya ya Newal, kukagua ujenzi wa ofisi mpya ya Halmashauri ya Mji wa Newala, kushiriki kupanda miche ya korosho katika kijiji cha Mtangalanga na kuzindua ugawaji wa pikipiki na guta kwa vikundi kupitia TAMOSA katika kijiji cha Chikunda Lubido.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa