• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Newala waja na mikakati ya kuboresha sekta ya elimu

Posted on: July 31st, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Newala Bi. Aziza Mangosongo amefanya kikao kazi na waratibu elimu kata pamoja na walimu wakuu wa shule za msingi na wakuu wa shule za sekondari za Wilaya ya Newala kwa siku mbili kuanzia tarehe 29 hadi 30 mwezi Julai, 2019.

Bi. Mangosongo ameitisha kikao hicho kwa lengo la kujadili maswala mbalimbali yanayohusu elimu na kupata mrejesho wa utekelezaji wa maagizo mbalimbali ya viongozi yakiwemo kumaliza ‘syllabus’ mapema ili kuwawezesha wanafunzi kufanya marudio na mitihani ya kujipima kwa wingi, kudhibiti utoro katika shule zetu, kubandika majina ya wanafunzi waliofanya vizuri kwenye mitihani ya Taifa katika mbao za matangazo za shule husika ili kuleta mori kwa wanafunzi wengine kufanya vizuri na uwepo wa bendera za Taifa katika shule zote za msingi na sekondari kwa kuwa hizo zote ni taasisi za Serikali.

Aidha, kikao hicho kilijadili pia maandalizi ya mitihani ijayo ya Taifa na Bi. Mangosongo amewataka walimu kuwapima wanafunzi kwa mitihani mbalimbali ya majaribio ili kujua uelewa wao na kufanyia kazi mada zote zinazoonekana kutoeleweka vizuri kwa wanafunzi wao.

Pia Bi. Mangosongo amewataka waratibu elimu kata kuwasaidia walimu wakuu katika kudhibiti utoro wa wanafunzi, kusimamia nidhamu kwa walimu na wanafunzi na kufuatilia na kusimamia miradiya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo ya shule ambayo imepatiwa fedha kutoka Serikalini. Aidha mafundi wote wanaopata kazi katika miradi hiyo lazima wawe na vitambulisho vya ujasiriamali vilivyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli.

Kikao hicho kilihitimishwa kwa walimu na waratibu elimu kata wote kuondoka na mikakati ya ufaulu ya kiwilaya ambayo ni kuwa na ushirikiano mkubwa baina ya walimu, kufanyika kwa vikao vya mara kwa mara vya walimu ili kujadili mafanikio na changamoto walizonazo katika utekelezaji wa majukumu yao na namna ya kutatua changamoto hizo, kufanyika kwa vikao vya kamati za shule, viongozi kutembelea kwenye shule mara kwa mara na kutoa ushauri, upatikanaji wa chakula shuleni ili wanafunzi wapate muda mwingi wa kujifunza, kuunda kwa kambi za wanafunzi kwa ngazi ya kata ili wanafunzi wabadilishane uzoefu na walimu washirikiane katika kufundisha na kumaliza ‘syllabus’ mapema.

Mikakati mingine iliyowekwa kwenye kikao hicho ni pamoja na kudhibiti utoro shuleni, kusimamia nidhamu kwa walimu na wanafunzi, kufanyika kwa mitihani ya kujipima ya mara kwa mara na utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wanaofanya vizuri ili kuleta motisha kwa wanafunzi wengine kutamani kufanya vizuri zaidi.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Kaimu katibu Tawala wa Wilaya ya Newala Bw. Lincolin Tamba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Newala Bw. Andrew Mgaya, Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bi. Nancy Lyimo, Kamanda wa TAKUKURU wilaya ya Newala Bw. Bernad Mkama, maafisa idara ya elimu msingi na sekondari, waratibu elimu kata, walimu wakuu wa shule za msingi na wakuu wa shule za sekondari zilizopo katika wilaya ya Newala.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa