• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

MILIONI 17.8 ZA MFUKO WA ELIMU ZATUMIKA KWA AJILI YA MOTISHA KWA WALIMU WALIOFANYA VIZURI KATIKA MASOMO YAO YA MADARASA YA MITIHANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA NEWALA

Posted on: February 19th, 2022

MILION 17.8 ZA MFUKO WA ELIMU NEWALA DC  ZATUMIKA MOTISHA

Halmashauri ya wilaya ya Newala Mkoa wa Mtwara imetumia shilingi milioni 17.8 kwa ajili ya utoaji wa tuzo kwa shule  na walimu waliofanya vizuri katika ufundishaji wa masomo ikiwa ni motisha baada ya wanafunzi  kufaulu vizuri mitihani ya taifa kwa mwaka 2021.

Utoaji wa tuzo hizo umefanyika leo katika sherehe iliyofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari Mnyambe ambapo shule bora 12 na walimu 88 wamepata zawadi ya vyeti na fedha.

Akizungumza katika sherehe hiyo mgeni rasmi  Merry Twamgabo, ambaye alimwakilisha Kaimu mkuu wa wilaya ya Newala amempongeza Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Newala kwa kuwapatia motisha walimu waliofanya vizuri katika ufundishaji na kwamba kitendo hicho  kitaleta hamasa zaidi ya walimu kujituma katika  ufundishaji .

Aidha ameipongeza kamati ya huduma za jamii kutenga fedha kupitia mfuko wa elimu kwa ajili ya kutoa  motisha ambapo amewataka walimu ambao wamekosa zawadi kujituma katika ufundishaji ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya taifa  mwaka 2022.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Newala, Famili Mshaghira amesema Halmashauri itaendelea kuunga mkono juhudi za walimu katika ufundishaji ambapo utaratibu wa kutoa motisha utaendelea kuwepo ili kuwapa hamasa ya kujituma. Amewataka walimu kushirikiana na kufanya kazi kwa weledi ili kuleta Matokeo chanya katika ufaulu wa wanafunzi.

Aidha kwa upande wake afisa elimu sekondari,Friday Sondasy, Halmashauri ya wilaya ya Newala amesema tuzo zilizotolewa zimezingatia katika upimaji wa mitihani ya darasani la 4,Matokeo ya elimu ya msingi ,upimaji wa mitihani ya kidato cha pili na matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2021.

Ameongeza kuwa zawadi ya vyeti na fedha zimetolewa kwa viongozi Bora ,shule Bora zilizo faulisha kwa 100% , walimu  waliofaulisha kwa 100%  na walimu waliofaulisha daraja A

Afisa Elimu Sondasy ametaja mikakati ya kuongeza ufaulu kuwa ni pamoja na kutoa motisha na kuzipitia shule zinazofanya vibaya ili kuzungumza na walimu kujua changamoto walikuwanazo na kuzitafutia ufumbuzi.

Sherehe za utoaji tuzo hii Leo zilihudhuliwa na wakuu wa shule,walimu wa taaluma ,walimu waliofanya vizuri,maafisa elimu kata ,maafisa Tarafa,wakuu wa idara,katibu wa chama Cha walimu na kamati ya ulinzi na usalama

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa