• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Mfuko wa Elimu furaha tele.

Posted on: June 20th, 2018

Bodi ya mfuko wa Elimu Wilayani Newala imeridhika na kufurahishwa na jitihada kubwa za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Elimu inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Newala kupitia mfuko wa Elimu.

Akizungumza mara baada ya ziara ya kutembelea miradi ya mfuko wa Elimu iliyofanyika tarehe 18/06/2018 katika shule za vijiji na kata tofauti tofauti Wilayani Newala, Mwenyekiti wa Bodi ya mfuko wa Elimu ya Halmshauri ya Wilaya ya Newala Mzee Mohamedi Abeid Liyanga, amesema bodi yake imeridhika na kufurahishwa na jitihada za hali ya juu za viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala katika kuhakikisha wanatekeleza ipasavyo miradi ya mfuko wa Elimu, ili iweze kusaidia kuboresha swala zima la Elimu bora kwa watoto waliodhamiria kusoma kwa bidii waweze kufaulu na kusonga mbele zaidi, na kwamba changamoto za kielimu zilizokuwa zinatokana na mapungufu ya baadhi ya miundombinu na kukosekana kwa huduma za msingi katika baadhi ya shule, zitakuwa zimetatuliwa.

Mzee Liyanga ameongeza kuwa, utekelezaji wa miradi hiyo unaonyesha dhahiri kuwa fedha za mfuko wa Elimu zilizotumika mpaka sasa, zinawiana vizuri na hali halisi ya hatua ya miradi ilipofikia, na hii inamaanisha kuwa ubora wa miradi hiyo umezingatia thamani ya pesa zilizokusudiwa.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa bodi hiyo amewashukuru wazazi na wananchi wa Newala hususani wale wa maeneo ya miradi husika, kwa kushirikiana vyema na serikali katika kuongeza nguvu ya utekelezaji wa miradi ya Elimu, ambayo ndiyo dira ya watoto katika Elimu na maisha yao ya baadae, amewaasa wazidi kuendelea kujitolea kushiriki katika ujenzi na uboreshaji wa shule mbalimbali ili kuinua kiwango cha Elimu Wilayani Newala.  

Awali shule mbalimbali za msingi na sekondari Wilayani Newala, zilionekana kukosa baadhi ya huduma za msingi kama vyoo na upungufu wa vyumba vya madarasa, jambo lililowaathiri wanafunzi wengi katika maendeleo ya taaluma na afya bora.

Ziara hiyo iliyowahusisha wajumbe wa bodi ya mfuko wa Elimu ya Halmashauri ya Wilaya ya Newala akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo, walifanikiwa kutembelea miradi mbalimbali ya Elimu ikiwemo ukarabati wa vyumba viwili vya madarasa shule ya sekondari Ushirika iliyopo Kata ya Mkwedu uliogharimu jumla ya shilingi milioni 7 mpaka sasa, mradi wa vyumba vitano (5) vya madarasa shule ya sekondari Makukwe ambao hadi kukamilika utagharimu shilingi milioni 80 na laki sita (80,600,000/=) ambazo zinatokana na michango ya wananchi kwenye mfuko wa Elimu kupitia makato ya mauzo ya zao la korosho,  ukaguzi wa ujenzi wa vyoo matundu manne shule ya msingi Mbuyuni iliyopo Kata ya Makukwe unaogharimu shilingi 2,518,000/= zilizotolewa na mfuko wa Elimu, mradi wa vyumba viwili (2) vya madarasa shule ya sekondari Vihokoli unaogharimu jumla ya shilingi milioni 30 laki 2 na elfu hamsini (30,250,000) ambapo kiasi ch shilingi 250,000/= ni michango ya wananchi wa Vihokoli, miradi mingine ni ujenzi wa vyoo matundu 6 na madarasa 2 shule ya sekondari Lengo,na umaliziaji wa ujenzi wa matundu 4 ya vyoo shule ya Msingi Lengo na umaliziaji wa ujenzi wa madarasa 2 na matundu 8 ya vyoo shule ya sekondari Malatu.

Mwenyekiti wa bodi ya mfuko wa Elimu Mzee Mohamedi Abeid Liyanga (aliyenyoosha mkono) akiwa pamoja na wajumbe wa bodi wakikagua ujenzi wa vyoo matundu 4 shule ya Msingi Mbuyuni iliyopo Kata ya Mkukwe tarehe 18/06/2018.

Wajumbe wa bodi ya mfuko wa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala wakikagua mradi wa ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa ya shule ya Sekondari Vihokoli Tarehe 18/06/2018.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa