• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Wilaya ya Newala yaadhimisha siku ya wanawake duniani

Posted on: March 9th, 2020

Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake (UWT) wa mkoa wa Mtwara Bi. Zuhura Farid  jana tarehe 08/03/2020 amewaongoza wakazi wa Newala katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani.

Maadhimisho hayo yalifanyika kiwilaya kwa wakina mama kushiriki katika shughuli za awali za ujenzi wa zahanati katika kijiji cha Nanguruwe kilichopo katika kata ya Nanguruwe Halmashauri ya mji wa Newala.

Pia wanawake wa Newala walifanya maandamano wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali kuhusu siku ya wanawake duniani ambayo yalianzia katika eneo la kituo cha mabasi Newala hadi viwanja vya mahakama ya mwanzo Newala mjini ambapo yalipokelewa na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Bi. Zuhura Farid akiwa na Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Newala  Bi. Aziza Mangosongo.

Akizungumza katika hotuba yake kwenye maadhimisho hayo, Bi. Zuhura Farid amewataka wanawake wazidi kushikamana, vikundi vya ujasiriamali wapewe elimu ya mapato na matumizi ili waweze kuendesha biashara zao vizuri pia wakipewa mikopo wafanye marejesho kama inavyotakiwa kwa kuwa Serikali ya awamu ya tano ikiongozwa na Rais John Magufuli inawasapoti wakina mama kwa kuwapa mikopo na wanarejesha bila riba.

Pia wanawake wa Newala walitakiwa kusheherekea siku hiyo kwa kuzingatia chanzo cha sherehe hizo ambacho ni kutetea haki za wanawake. Pia wanawake wametakiwa kuzingatia maadili kwao na katika malezi kwa kuzungumza na watoto mara kwa mara, kutumia lugha nzuri katika mawasiliano, kujenga urafiki na walimu ili kujua mienendo ya watoto wao shuleni.

"Nasisitiza jamii kubadili fikra hasi juu ya wanawake na kudumisha usawa wa kijinsia." Alisema Bi. Zuhura Farid.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kwa mwaka huu 2020 ni "Kizazi cha usawa kwa maendeleo ya Tanzania ya sasa na ya baadaye".


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa