• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Watumishi Newala watakiwa kuwa wabunifu na kuhakikisha ulinzi na usalama wa watu wao.

Posted on: July 13th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Mwangi Rajab Kundya leo tarehe 13/07/2021 amekutana na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo ualimu Kitangari. 

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Mwangi Rajab Kundya akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Kundya amewataka watumishi hao kuwa wabunifu katika utendaji wao wa kazi kwa kuhakikisha kazi zao zinaleta matokeo bora kwa jamii katika kipindi chote wanachowatumikia wananchi.

"Utendaji wako wa kazi hautapimwa kwa  kuwepo kwako kazini kwa muda mrefu au wingi wa vyeo ulivyowahi kushika, bali utapimwa kwa matunda bora yaliyopatikana katika kipindi chako ulichokuwa kazini." Alisema Mhe. Kundya. 

Pia Mhe. Kundya ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha watumishi kuwa ugonjwa korona upo hivyo wafanye kazi huku wakichukua tahadhari kwao na kwa watu wanaoshi nao kwa kuwa na utaratibu wa kuweka sehemu za kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni ili kujiepusha na virusi hivyo ya korona.

"Nawakumbusha ugonjwa wa korona upo, twendeni tukafanye kazi ya kuwazoesha watu tunaowaongoza kuishi kwa tahadhari kwa kujenga tabia ya kuosha mikono kwa maji tiririka na sabuni, kuepuka mikusanyiko mikubwa isiyo na lazima.........kuwawezesha watu wetu kuzifahamu dalili za korona ili akimuona mtu mwenye dalili hizo amshauri haraka kuwaona wataalam wa afya."

"Nawaomba na kuwasihi katika ofisi zetu, katika shule zetu tuanzishe utaratibu wa kuwa na sehemu za kuosha mikono kwa maji tiririka na sabuni, tukifanya hivyo tutaepuka na korona na magonjwa ya tumbo na kuharisha." Alisema Mhe. Kondya. 

Wakati huo huo, Mhe. Kondya pia amewataka watumishi hao kushiriki katika kuhakikisha ulinzi na usalama wa jamii zetu kwa kuimarisha mfumo wa ulinzi kwa jamii ili pale watakapohisi kuna uvunjifu wa amani waweze kutoa taarifa mapema katika vyombo vya ulinzi na usalama.

Pia watendaji wa vijiji wametakiwa kuyatumia madaftari ya wakazi kwa kuwaandikisha kila mtu anayefika kuishi katika eneo lake la utawala na kujua shughuli wanazofanya wakazi wa maeneo yao.

Kikao hicho cha Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Newala kimehudhuriwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Newala Bw. Daniel Zenda, wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Newala, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Mhe. Tamimu Ladda, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Duncan Thebas, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Watendaji Kata, Waratibu elimu kata, Wakuu wa Vituo vya afya na zahanati na watendaji wa vijiji.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa