• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

UKOSEFU WA MASOKO NA PUNGUZO LA VIWANGO VYA UTOZAJI WA USHURU KUPUNGUZA MAPATO YA NDANI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA

Posted on: November 2nd, 2017

Mapato ya ndani ni moja ya vyanzo vya mapato vinavyoisaidia Halmashauri ya Wilaya ya Newala kujiendesha yenyewe kwa kuwezesha shughuli mbalimbali za idara na vitengo vya Halmashauri na miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi wa Wilaya ya Newala.

Kwa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, ushuru wa mazao mchanganyiko ni moja kati ya vyanzo vikuu vya mapato. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018, hali ya ukusanyaji mapato ya ushuru wa mazao mchanganyiko hasa mbaazi imeathirika kutokana na kukosa soko la zao hilo. Hali hii imesababisha wakulima kushindwa kuuza mazao yao na hivyo kupelekea kushindwa kupata ushuru unaotokana na zao hilo.

Akizungumza na wananchi kupitia baraza la madiwani lililofanyika tarehe 02/11/2017, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae alieleza kupungua kwa mapato hayo kwa robo hii ya kwanza ya mwaka 2017/2018  kwa kulinganisha na robo ya kwanza ya 2016/2017 ambapo kwa robo hiyo ya mwaka 2016/2017 Halmashauri ilikuwa imekusanya Tsh. 118,742,500.00 zilizotokana na zao hili na kwa robo hiyohiyo kwa mwaka huu jumla ya makusanyo ni Tsh. 12,305,310.00 yakiwa na tofauti kubwa ya Tsh. 106,437,190.00.


Aliendelea kusisitiza kuwa, kupungua kwa viwango vya utozaji wa ushuru wa mazao mchanganyiko kutoka asilimia tano (5%) hadi asilimia tatu (3%) kwa mazao ya biashara na asilimia mbili (2%) kwa mazao ya chakula pia kumeathiri kwa kiasi kikubwa bajeti ya Halmashauri kwa kuwa tayari ilikwisha andaliwa kwa kuzingatia ushuru wa asilimia tano (5%). Bw. Chimae alisema kuwa hali hii itaathili pia sehemu ya shughuli ambazo zilitakiwa zitekelezwe kwa kutumia mapato ya ndani.

Hata hivyo ili kuendana na hali halisi ya mapato, Halmashauri inatarajia kupitia upya makisio ya mapato ya ndani ili yaendane na ada mpya za ushuru ifikapo mwezi  Disemba, 2017.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa