• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Sekondari ya Mkoma II Halmashauri ya Wilaya ya Newala yaja na mkakati wa kuongeza ufaulu na kukuza taaluma kwa wanafunzi

Posted on: July 9th, 2020

Wakazi wa kata ya Mkoma II na Nambali leo tarehe 09/07/2020 wamekubaliana kujenga bweni kwa ajili ya watoto wa kike katika shule ya Sekondari Mkoma ili kukomesha utoro na kukuza ufaulu kwenye mitihani.

Baadhi ya wazazi na wakazi wa kata ya Mkoma II na Nambali wakiwa kwenye mkutano na uongozi wa shue kujadili ujenzi wa bweni la wasichana shuleni hapo leo.

Makubaliano hayo yamefanyika katika mkutano wa wazazi na uongozi wa shule uliofanyika shuleni hapo ambapo wazazi wa kata zote mbili za Mkoma II na Nambali ambazo zinahudumiwa na shule hiyo wamekubaliana kuchangia shilingi elfu tano kwa kila kaya ambapo wanatarajia kukusanya jumla ya shilingi milioni kumi kwa ajili ya kuanza ujenzi huo ifikapo tarehe 31/08/2020.

Mkuu wa shule ya sekondari Mkoma II Bw. Daniel Lukuwi akizungumza na waliohudhuria mkutano wa kujadili ujenzi wa bweni la wasichana kwa lengo la watoto hao kukaa shuleni.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Shule ya Sekondari Mkoma Bw. Daniel Lukuwi amesema kuwa, wazo la shule hiyo kujenga bweni kwa ajili ya wasichana limekuja baada ya wanafunzi wengi hasa wa kike kuwa watoro, kuacha shule na wengine kuahirisha masomo.

"Ufaulu wa wanafunzi unashuka sana kwa kuwa jamii hii ni ya kilimo cha kuhama, hivyo msimu wa kilimo cha ufuta wazazi huama makazi yao na kwenda Liwale Lindi, watoto wanaachwa bila usimamizi hivyo kupelekea baadhi kuwa watoro na watoto wengine husafiri na wazazi kwenda shambani hivyo kusimama masomo." Alisema Mwalimu Lukuwi.

Wakizungumza katika mkutano huo, wazazi waliupongeza uongozi wa shule kwa kuja na wazo la kujenga hosteli kwa kuwa itawasaidia watoto kubaki shuleni kipindi ambacho wazazi wanasafiri kwenda kulima ufuta mkoa wa Lindi.

Mkutano huo uliwahusisha wazazi na walezi wa wanafunzi, uongozi wa shule na, uongozi wa kata na vijiji pamoja na uongozi wa Halmashauri ambao uliwakilishwa na Afisa Elimu Sekondari Bw. Friday Sondasy na Afisa Ardhi na Maliasili Bi. Magreth Likonda ambapo jamii ya kata ya Mkoma II na Nambali iliahidi kuchangia kwa kila kaya na jumla ya shilingi laki tano na sitini na tano na ahadi ya mifuko kumi ya saruji zilitolewa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa