• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Newala na Masasi watakiwa kuheshimu mipaka ya ardhi iliyowekwa awali

Posted on: July 28th, 2021

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula leo Jumatano tarehe 28/07/2021 amewataka wakazi wa Newala na Masasi kuheshimu mipaka ya ardhi iliyowekwa ili kuepuka migogoro ya ardhi.

Mhe. Mabula ameyasema hayo katika kijiji cha Miyuyu, kata ya Chilangala, Wilaya ya Newala alipofika kusikiliza na kutatua mgogoro wa uhalisia wa mpaka wa ardhi kati ya Newala na Masasi unaotenganisha kijiji cha Miyuyu kilichopo Newala na kijiji cha Ndanda kilichopo Masasi.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi, Mhe. Angeline Mabula (wa kwanza kushoto) akipitia tangazo la Serikali kuhusu mpaka wa Newala na Masasi

Akizungumza katika ziara hiyo, diwani wa kata ya Chilangala Mhe. Nandonde Jamali Jaffu ameeleza kuwa malalamiko ya wananchi ni kuwa mipaka ya asili (ya kichifu) haikuzingatiwa wakati wa kuandaa ramani za vijiji na kuweka mipaka ya Wilaya hivyo wananchi hawakubaliani na mipaka iliyopo kwenye ramani. 

Aidha, Mhe. Mabula ameelekeza Wakurugenzi kwenda kwenye maeneo yote yenye migogoro na kuwasilikiliza wananchi kujua changamoto yao ni nini, na wakishakubaliana, ofisi ya ardhi itatekeleza kwa kuweka mawe ya mipaka kwa mujibu ya makubaliano yao.

"Naagiza Wakurugenzi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala na Halmashauri ya Mji Masasi kwenda kwenye vijiji vyenye migogoro kuwakutanisha wananchi wa vijiji husika vilivyopo mpakani, chukueni ramani na tangazo la Serikali (GN) lililotolewa la vijiji husika na muwasomee ili waelewe vizuri". Alisema Mhe. Mabula. 

Mhe. Mabula amewaeleza wananchi kuwa mipaka haiwazuii wananchi kufanya shughuli zao za kiuchumi ilimradi watafuata taratibu zote za matumizi bora ya ardhi yaliyowekwa katika eneo husika.

Mhe. Mabula ameeleza kuwa, mipaka inayotambulika kwa sasa ni ile iliyopo kwenye ramani na iliyotolewa kwenye tangazo la Serikali na iwapo wananchi watataka marekebisho wanatakiwa kufuata taratibu za awali zilizotumika kuandaa mipaka hiyo.

Ziara hiyo ya Mhe. Mabula ni utekelezaji la agizo lililotolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Mpango alilolitoa akiwa kwenye ziara Wilayani Newala siku ya Jumapili tarehe 25/07/2021 akimuagiza Mhe. Mabula kubaki Newala ili kushughulikia mgogoro wa ardhi uliowasilishwa na Mbunge wa jimbo la Newala Vijijini Mhe. Maimuna Mtanda.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa