• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

NEWALA DC YAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA AFUA YA LISHE ROBO YA KWANZA 2024/25

Posted on: November 15th, 2024

NEWALA MTWARA

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Rajabu Kundya amewaasa watendaji kata wa Newala DC kuchagua viongozi Bora katika uchaguzi wa serikali za mitaa,ambao watakuwa mstari wa mbele katika kuhimiza na kusimamia utekelezaji wa Afua bora za lishe katika Jamii.


 Mhe. Kundya amesema hayo jana Novemba 14,2024 katika kikao cha Tathmini ya utekelezaji wa Afua za lishe robo ya kwanza 2024/25 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri na kuhudhuriwa na wajumbe wakiwemo wakuu wa idara na vitengo,Mkurugenzi mtendaji ,watendaji kata,Wasimamizi wa shughuli za Afya na Viongozi wa Serikali.


 " Upo uhusiano baina ya kura na lishe, maana mpango wetu wa utekelezaji wa Afua za lishe unategemea na ufanisi wa viongozo watakaochaguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa 27 Novemba 2024"

 "Wao ndio watawakabili wananchi kwa hili na lile ili wachangie chakula na kuleta mafanikio katika suala la lishe,hivyo kama tukifanya makosa kwenye uchaguzi huu tukapata viongozi wa hovyo,basi mtaona mambo yetu yataendela kukwama zaidi na kutuingiza katika janga la watoto wetu kupata udumavu na athari nyingine zitokanazo na Lishe" amesema Kundya.


Aidha  taarifa ya tathmini iliyowasilishwa na Afisa Lishe Halmashauri ya wilaya ya Newala, Bi. Jane Mgaza,imebainisha mafanikio ya hali ya lishe ambapo katika ipimaji wa Kadi ya alama ya kijani, kata nyingi zimetekeleza Afua za Lishe kuanzia asilimia 80-100.


Mhe Kundya amepongeza mafanikio hayo na kuendelea kutoa msisitizo kwa timu ya Lishe kwenda kuhamasisha Jamii kuchangia chakula shuleni ili watoto wote wapate chakula wakiwa shuleni na pia  ameelekeza  watendaji kata ambao kata zao hazijafanya vizuri katika utekelezaji wa afua za lishe kwenda kuhamasisha zaidi wananchi kuzingatia ulaji wa lishe Bora .


Kupitia taarifa ya Tathmini ya utekelezaji wa shughuli za Afua za lishe robo ya kwanza ya mwaka wa fedha  2024/25,Kitengo cha Afya na Lishe kimefanikiwa  kutembelea na kutoa Elimu ya Lishe vijiji 30 katika maadhimisho ya siku ya Lishe na Afya ya Kijiji (SALIKI), kutoa mafunzo ya  Lishe kwa watendaji 22 na maafisa Tarafa 4 na watoa huduma za lishe katika vituo vyote vya kutolea huduma .

@ortamisemi

@mtwarars_habari

@dc_newal

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa