• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara afanya ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Newala

Posted on: May 11th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amefanya ziara ya kusikiliza kero, changamoto na maoni kutoka kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala siku ya Ijumaa tarehe 10/05/2019 kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi ya kata ya Kitangari, Wilaya ya Newala.

Kupitia mkutano huo, mkuu wa mkoa ameweza kupokea kero na changamoto mbalimbali za wananchi  zikiwemo ucheleweshwaji wa utoaji wa hukumu za kesi katika mahakama ya mwanzo, tabia za wafanyabiashara kuuza dawa za kupulizia mikorosho kiholela, madai ya fedha za uzalishaji wa miche ya mikorosho kwa msimu wa mwaka 2017/2018, madai ya baadhi ya wakulima wa chama cha msingi Chemana kuhusu malipo ya korosho za msimu wa 2017/2018, upimaji wa ardhi, ukosefu wa maji, ukosefu wa umeme na ubovu wa miundombinu ya barabara huku wakuu wa idara husika wakitakiwa kutoa majibu na ufafanuzi juu ya kero na changamoto hizo.

Akiendelea kuzungumza na wananchi wa Newala, Byakanwa amewataka wajasiriamali kuwa na vitambulisho vya ujasiriamali vilivyotolewa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Joseph Magufuli. "Mhe Rais amekusudia kuwasaidia wajasiriamali wenye kipato cha chini ambao faida inayotokana na biashara zao haifikii shilingi milioni nne kwa mwaka kwa kuwapatia vitambulisho vya ujasiriamali ili kuwaondolea hali ya ulipaji wa kodi za mara kwa mara na badala yake walipie shilingi elfu ishirini tu kwa mwaka" alisema Byakanwa.

Mikutano hiyo ya kusikiliza kero ni moja ya njia anayoitumia Byakanwa kukutana na wananchi wa mkoa wake na kushughulikia matatizo waliyonayo ikiwa pia ni utekelezaji wa agizo la Mhe Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa viongozi wa mikoa yote kuzifahamu na kusaidia kutatua kero za wananchi.





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa