• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala watakiwa kuwatumikia wananchi wa Newala kwa uaminifu.

Posted on: December 5th, 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Newala siku ya jana Ijumaa, tarehe 04/12/2020 imefanya mkutano wake wa kwanza wa baraza la madiwani tangu ufanyike Uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani mwezi Oktoba mwaka huu 2020.

Akizungumza katika mkutano huo wa baraza la madiwani, mgeni rasmi katika mkutano huo ambaye ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw. Alphayo Kidata alianza kwa kuwaeleza madiwani juu ya uhusiano wa kimadaraka na kimajukumu kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kwa lengo la kumuhudumia mwananchi wa kawaida.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw. Alphayo Kidata (aliyesimama) akizungumza katika mkutano wa baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Kutoka upande wa kushoto ni Mbunge wa jimbo la Newala Mhe. Maimuna Mtanda,  na kulia ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Mhe. Ladda Mfaume Tamimu.

Pia Bw. Kidata aliwakumbusha madiwani majukumu yao ya msingi wanayotakiwa kuyafanya kama wawakilishi wa wananchi.

"nyinyi mmetumwa na wananchi, wamewachagua, kwa hiyo nyinyi ni wawakilishi wa wananchi wote wa kata zenu katika Halmashauri hii. Kwa njia hiyo na msingi huo, hoja zozote utakazokuwa unazileta Mheshimiwa diwani kwenye baraza la Halmashauri ni hoja ambazo umeshirikishana na wananchi wako wakakutuma uzilete na siyo ulete hoja zako binafsi." Alisema Bw. Kidata.

Bw. Kidata pia amewataka madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala kuwa waaminifu katika kipindi chote cha utawala wao kwa kuwa wananchi wa jimbo la Newala vijijini wana imani sana nao na wamewakabidhi ndoto zao, na hilo ni deni kubwa sana kwao.

Aidha, Mhe. Mbunge wa jimbo la Newala vijijini Bi. Maimuna Mtanda pia alitumia mkutano huo wa baraza la madiwani kuwashukuru wananchi wa jimbo la Newala vijijini wote kwa kukiamini Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kumchagua kwa kishindo Mhe. Rais, yeye Mbunge pamoja na waheshimiwa madiwani.

"Tunawashukuru wana Newala wote kwa kazi nzuri, kwanza wamempa kura nyingi Mhe. Rais, lakini pia kwa kukiamini Chama Cha Mapinduzi na kukipa ushindi uliotukuka." Alisema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda ameahidi kuwa yeye na waheshimiwa madiwani watatoa ushirikiano wa kutosha katika maeneo yote kwa viongozi wa dini, watumishi wa umma na wananchi wote ambao wanatakiwa kuwahudumia.

Wakati huohuo, Mkuu wa Wilaya ya Newala, Mhe. Aziza Mangosongo amewataka waheshimiwa madiwani wote kusoma vizuri kanuni, sheria na taratibu za Halmashauri na kutekeleza majukumu yao kwa kutekeleza vyema ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

"Haijalishi wewe ni mwanachama wa chama gani, hapa tunataka wewe utekeleze ilani ya chama kinachotawala, Chama Cha Mapinduzi." Alisema Mhe. Mangosongo.

Mhe. Mangosongo pia amewataka madiwani wote kwenda kuanzisha miradi mipya ya maendeleo na kuiendeleza miradi ya zamani katika kata zao.

"Tusibuni wenyewe miradi kichwani, tuwashirikishe wananchi na watendaji katika kata zetu." Alisisitiza Mhe. Mangosongo.

Mkutano huo wa baraza la madiwani umefanyika kwa siku moja katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha walimu Kitangari  na ulihudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Duncan Thebas, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw. Alphayo Kidata, Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo, wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Newala, Mhe. Mbunge wa jimbo la Newala vijijini Bi. Maimuna Mtanda, viongozi wa vyama vya siasa vya CCM na ACT wazalendo wilaya ya Newala, viongozi wa dini,maafisa wa Maadili Sekretariet ya Maadili ya viongozi wa umma kanda ya Kusini, Hakimu Mkazi wa wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Nasra Mkadam Mwinshehe, waheshimiwa madiwani, wakuu wa idara na vitengo, wageni waalikwa na waandishi wa habari.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa