• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Kampeni ya "Shule ni Choo" yapata muitikio mkubwa Newala

Posted on: September 21st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe.Gelasius Byakanwa ametambulisha rasmi kampeni ya "Shule ni Choo" kwa Wilaya ya Newala siku ya Ijumaa tarehe 20/09/2019.

Kampeni hiyo ya "Shule ni Choo" ni njia anayoitumia Mhe. Byakanwa kuhakikisha vinajengwa vyoo vya wanafunzi na walimu kwenye shule zenye uhaba wa vyoo kwa kutumia michango inayotolewa na wadau mbalimbali wakiwemo watumishi wa umma waliopo kwenye maeneo husika, viongozi, wakuu wa taasisi mbalimbali na wananchi wote.

Akitambulisha kampeni hiyo, kwenye kikao na watumishi, madiwani wa Halmashauri wa Wilaya na Mji wa Newala, wakuu wa taasisi mbalimbali na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya, Mhe. Byakanwa ameeleza kuwa katika baadhi ya maeneo ambapo zimejengwa shule, vimejengwa vyumba vya madarasa tu badala ya majengo yote yanayohitajika ili kukidhi uwepo wa shule. Hivyo ameamua kuja na kampeni hiyo baada ya kuona uhaba mkubwa wa matundu 6547 ya vyoo vya wanafunzi na 1830 ya vyoo vya walimu kwenye shule za msingi zilizopo kwenye mkoa wote wa Mtwara.

Katika kuunga mkono kampeni ya "Shule ni Choo" jumla ya ahadi za shilingi milioni kumi na laki tatu pamoja na mifuko mia sita na sabini na tisa ya saruji zilitolewa katika harambee iliyoitishwa na Mhe. Byakanwa kwenye kikao hicho.

Mbali na kampeni hiyo, Mhe. Byakanwa pia alisisitiza juu ya utekelezaji bora wa sheria ya mipango miji, kuujenga mji wa Newala na kuwekeza katika sekta mbalimbali, na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 24/11/2019.
Kampeni ya "Shule ni Choo" inatarajiwa kuzinduliwa rasmi tarehe 12/10/2019 Mkoani Mtwara na mgeni rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa