• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Wasimamizi wasaidizi na waandikishaji wa wapiga kura Newala watakiwa kufuata kanuni

Posted on: October 6th, 2019

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na waandikishaji wa wapiga kura wametakiwa kufuata kanuni zinazowaongoza ili kufanikisha majukumu yao.

Hayo yamesemwa na Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo wakati akifungua mafunzo ya wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na waandikishaji wa wapiga kura wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala siku ya Jumamosi tarehe 05/10/2019.

Mkuu wa Wilaya ya Newala, Mhe. Aziza Mangosongo akizungumza wakati akifungua mafunzo ya wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na waandikishaji wa wapiga kura.

Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Mhe. Mangosongo amewaeleza wasimamizi na waandikishaji hao kuwa, Serikali imewaamini na kuwapa dhamana hiyo, hivyo wafuate kanuni zinazowaongoza ili kutoiingiza hasara Serikali.

"Uteuzi wenu umezingatia kanuni za Serikali za mitaa kifungu namba 7(1) na kifungu namba 10(2), ninawaasa kuwa mkafanye kazi hii kwa uaminifu mkubwa, mkizingatia kanuni zinazowaongoza katika kufanya kazi hiyo" alisema Mhe. Mangosongo.

Mafunzo hayo yameambatana na kuapishwa kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi 129 na waandikishaji wa wapiga kura 302 walioweka kiapo chao mbele ya Mhe. Hakimu Mkazi Glory Mwakihaba.

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na waandikishaji wa wapiga kura wakiapa kiapo cha uaminifu katika kutekeleza majukumu yao.

Uandikishaji wa wapiga kura unatarajiwa kufanyika kwa siku saba kuanzia Jumanne tarehe 08 hadi tarehe 14/10/2019 katika vitongoji vyote 302 vya Halmashauri ya Wilaya ya Newala.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa