Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Uzinduzi wa ugawaji dawa za kichocho na minyoo ya tumbo kwa watoto wa shule za msingi umefanyika leo Newala.

Posted on: May 20th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Newala Newala Mhe. Aziza Mangosongo leo tarehe 20/05/2021 amezindua rasmi zoezi la ugawaji wa dawa za kichocho na minyoo ya tumbo kwa watoto wa shule za msingi zilizopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwenye shule ya msingi Chiwonga.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mratibu wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele, Dkt. Hamis Mpoteni amesema kuwa zoezi hilo la ugawaji wa dawa za kichocho na minyoo linafanyika katika shule zote za msingi zilizopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

"Zoezi hili linafanyika katika shule zote za msingi 76 zilizopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Newala ikiwa ni muendelezo wa utoaji kinga tiba ambao hutolewa kila mwaka kwa lengo la kuwakinga na kuwatibu watoto na magonjwa ya kichocho na minyoo ya tumbo ambayo hayapewi kipaumbele na jamii licha ya kuwa na athari kubwa kwa watoto hasa upande wa ukuaji wa mwili na akili". Alisema Dkt. Mpoteni.

Dkt. Mpoteni ameeleza kuwa magonjwa hayo ni hatari kwa kuwa yanaweza kusababisha vifo japo yanaweza kuzuilika kwa kuzingatia usafi wa mikono na mwili; usafi wa choo na mazingira; kujiepusha kuoga, kuogelea na kutembea bila viatu kwenye maji yaliyotuama; kutibiwa haraka mara baada ya kuona dalili au kugundulika na magonjwa hayo.

Akizindua zoezi hilo, Mhe. Mangosongo  amewataka wazazi kuzingatia usafi kwao na kwa watoto wao na kuwa magonjwa yote yana madhara kama hayajapatiwa tiba na kinga kwa wakati.

"Madhara ya kutozingatia kinga na tiba ya magonjwa ya minyoo ya tumbo na kichocho ni kupata kansa ya kibofu, ugonjwa wa minyoo utakaosababisha madhara kwenye utumbo, kupungukiwa damu mwilini na mama mjamzito kuzaa mtoto mwenye udumavu." Alisema Mhe. Mangosongo.

Aidha wakati huo huo, wakazi wa Chiwonga walipata fursa ya kupewa elimu ya lishe bora na malezi.

Zoezi hilo lilizinduliwa kwa watoto kupatiwa dawa hizo na litaendelea kutolewa katika shule zote za msingi zilizopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Wazazi wa watoto hao walitumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali kwa kuwaletea huduma hiyo kwani inasaidia kuwakinga watoto wao na magonjwa hayo.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Newala, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Mhe. Isabela Makumbuli, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Bw. Friday Sondasy, Diwani wa kata ya Chiwonga Mhe. Kazumari Nauma, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Dkt. George Matiko, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala na wananchi wa kijiji cha Chiwonga.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa