• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Utawala bora waendelea kuimarishwa Newala

Posted on: August 25th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo jana siku ya Jumatatu tarehe 24/08/2020 amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Chilondolo kata ya Mtopwa, Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Mkutano huo ni muendelezo wa ziara za Mhe. Mangosongo katika vijiji vya Newala ili kusikiliza na kutatua kero za wananchi na aliwataka wakazi wa Chilondolo kutoa kero walizonazo ili azifanyie kazi kwa maendeleo ya Newala.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano huo, wakazi wa Chilondolo wamemueleza Mhe. Mangosongo juu ya uchakavu wa miundombinu ya majengo ya shule ya msingi Mtopwa; ubovu wa barabara ya kutoka Mtopwa kupitia Chilondolo hadi Tulieni; kukosekana kwa zahanati katika kijiji chao na kufanya wakazi wa hapo kupata huduma za afya katika kijiji cha Mnyeu ambapo ni mbali kutoka katika makazi yao; uchache wa virura vya kuchotea maji; upewaji wa kipaumbele kwenye matibabu kwa wazee; upatikanaji wa vitambulisho vya Taifa na kutaka Serikali iwasaidie kutatua kero hizo.

Aidha kutokana na hoja hizo, Mhe. Mangosongo aliwaruhusu wataalam wanaohusika na sekta zenye hoja hizo kutoa ufafanuzi na majibu kwa wananchi na baadaye alitoa maelekezo kwa wataalamu hao kwa ajili ya utekelezaji.

Mhe. Mangosongo kwa upande wa miundombinu ya majengo yakiwemo ya shule na zahanati, aliwataka wakazi wa Chilondolo kuanza ujenzi wa miundombinu hiyo kwa nguvu zao wenyewe na baadaye Serikali itawasaidia kumalizia baada ya wao kufikia hatua ya lenta katika ujenzi huo. Aidha, kuhusu miundombinu ya matundu manne ya vyoo ambavyo vimeshaanza kujengwa kwa nguvu za wananchi, Mhe. Mangosongo ameahidi kuwapatia vifaa katika ujenzi huo baada ya kufikia vigezo vinavyotakiwa vya mradi wa shule ni choo.

Kwa upande wa ukarabati wa barabara, Mhe. Mangosongo amewataka wakala wa barabara vijijini (TARURA) kuanza uchongaji wa barabara hiyo mara moja kwa kuwa wamemuahidi kuwa imewekwa kwenye mpango wa matengenezo ya mwaka huu wa fedha 2020/2021, pia wataalamu wa wakala wa maji vijijini (RUWASA) kufika kijijini hapo ndani ya wiki hii kufanya tathmini ya namna ya kuongeza vilula vya kuchotea maji.

Kwa upande wa vitambulisho vya Taifa, wananchi wa Chilondolo wametakiwa kuwasilisha taarifa sahihi NIDA pale yanapohitajika marekebisho ili kuondoa tatizo la taarifa zao kutoshabihiana na kupelekea vitambulisho vyao kutopataikana kwa wakati.

Pia, Mhe. Mangosongo ameitaka idara ya afya kuhakikisha wamemuweka muhudumu atakayewapa maelekezo wazee pindi wanapofika kupata huduma za afya ili wapate huduma hiyo kwa haraka.

Mhe. Mangosongo katika mkutano huo aliongozana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya,  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Bi. Magreth Likonda na wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • NEWALA DC YATOA SHUKRANI KWA MHE.RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

    June 04, 2025
  • Utekezaji wa Ujenzi mpya ya Sekondari Mtunguru

    May 29, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA

    May 29, 2025
  • UTEKEZAJI WA ILANI YA CCM

    May 27, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa