RAIS SAMIA AWASUKUMA NEWALA DC KWENYE NISHATI SAFI :MAJIKO YA GESI kWA BEI YA RUZUKU
Imeandikwa na Afisa Habari Shabani Mkumba.
Serikali kupitia Mradi wa Taifa wa Nishati Safi kwa Kupikia unaoratibiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imeipatia Halmashauri ya Wilaya ya Newala jumla ya mitungi 1,780 ya gesi ya kupikia, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maono ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wanatumia nishati salama na rafiki kwa afya na mazingira.
Akizungumza leo Juni 23, 2025 katika ofisi ya Halmashauri wakati wa zoezi la ugawaji wa mitungi hiyo kwa wananchi, Afisa Usafi na Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Ndugu.Tumaini Sadick, alisema kuwa utekelezaji wa mpango huo ni hatua muhimu katika kupunguza matumizi ya kuni na mkaa ambayo yamesababisha athari za kiafya na kimazingira kwa muda mrefu.
“Kupitia mradi huu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, Halmashauri ya Newala tumepokea mitungi 1,780 ya gesi kwa ajili ya wananchi. Mitungi hii inatolewa kwa bei ya ruzuku ambapo mwananchi anachangia shilingi 19,500 na serikali inachangia kiasi hicho hicho, hivyo kufanya gharama kuwa shilingi 39,000 tu kwa kila jiko,” alisema Ndugu Sadick.
Alieleza kuwa mitungi hiyokutoka Kampuni ya Taifa Gesi imeanza kugawiwa kwa wananchi waliopo kwenye mpango huo katika vijiji mbalimbali, kwa kushirikiana na kitengo cha maliasiri na hifadhi za mazingira huku elimu ya matumizi salama ya gesi ikiendelea kutolewa.
Ndugu. Sadick alisisitiza kuwa matumizi ya gesi yatasaidia kulinda au kupunguza magonjwa dhidi ya moshi unaotokana na kuni, sambamba na kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa.
Aidha, alitoa shukrani kwa Serikali kwa kuwezesha upatikanaji wa majiko haya kwa ruzuku, akisema kuwa hatua hiyo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wa vijijini wanaotegemea kuni kama chanzo kikuu cha nishati ya kupikia.
@mtwarars_habari
@samia_suluhu_hassan
@msemajimkuuwaserikali
@ortamisemi
@dc_newala
https://www.instagram.com/p/DLQfrctooQr/?igsh=aHRscGl4enN1OHMz
Kitangari,Newala
Anuani ya Posta: P.O. Box 16
Simu: +255232410251
Mobile:
Barua pepe: ded@newaladc.go.tz
Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa