Halmashauri ya Wilaya ya Newala ilifanya kikao maalum cha kuvunja Baraza la Madiwani mnamo Juni 20, 2025, katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo. Kikao hicho kilifanyika kufuatia kumalizika kwa muda wa uhai wa Baraza hilo la miaka mitano (2020–2025), kama inavyoelekezwa na kanuni za Serikali za Mitaa.
Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri, Mheshimiwa Mfaume Tamimu Ladda, na kuhudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Duncan Thebas, Mkuu wa Wilaya Mhe. Rajabu Kundya, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Waheshimiwa Madiwani pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo.
Mhe. Ladda aliwapongeza madiwani kwa ushirikiano walioutoa katika kipindi chote cha uongozi na kusema kuwa mafanikio yaliyopatikana yametokana na mshikamano wa pamoja kati yao na watendaji. “Tumefanya kazi kubwa kwa pamoja. Tumeboresha huduma kwa wananchi na kusimamia miradi ya maendeleo kwa ufanisi,” alisema.
Alihitimisha kwa kuwahimiza madiwani hao kuendelea kuwa sehemu ya harakati za maendeleo hata baada ya kumaliza muda wao wa uongozi.
Kitangari,Newala
Anuani ya Posta: P.O. Box 16
Simu: +255232410251
Mobile:
Barua pepe: ded@newaladc.go.tz
Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa