• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Mhe. Magufuli aweka jiwe la msingi ujenzi wa kuboresha miundombinu ya chuo cha ualimu Kitangari, Newala

Posted on: April 4th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli amefanya ziara ya siku moja Wilaya ya Newala siku ya Jumatano tarehe 03/04/2019.

Ziara hiyo ilihusisha kuwasalimia wananchi wa Newala na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa kuboresha miundombinu ya chuo cha ualimu Kitangari.

Akimkaribisha Mhe. Rais Magufuli katika chuo cha ualimu kitangari, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Ndalichako alieleza kuwa chuo hicho kilianza rasmi mwaka 1937 kama shule na mwaka 1975 kilibadilishwa na kuwa chuo cha ualimu.

Mradi huo wa ujenzi wa kuboresha miundombinu ya chuo ulianza mwezi Julai 2016 na unahusisha  ujenzi wa kumbi za mihadhara, mabweni ya wanafunzi, maabara, madarasa, ofisi na visima vya maji. Mradi huo unagharimu jumla ya shilingi bilioni nane na milioni mia mbili na sitini na tisa ambapo fedha za mradi huo zimetolewa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Canada.

Akizungumza na wakazi wa Newala, Mhe. Rais Magufuli alianza kwa kuwashukuru wana Newala kwa kumpa kura za kutosha kumfanya awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na aliwahakikishiwa kuwa atawalipa kwa kuwafanyia kazi.

Pia Mhe. Rais Magufuli aliishukuru Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kumualika kuja kuweka jiwe la msingi katika chuo cha ualimu Kitangari ikiwa ni utekelezaji wa ahadi alizozitoa za kuendeleza elimu ikiwa ni pamoja na kutoa elimu bure, mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, kuboresha miundimbinu ya shule na kukarabati na kuendeleza miundombinu ya vyuo vya ualimu.

Akiendelea kuzungumza na wakazi wa Newala, Mhe. Rais Magufuli alitumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali ya Canada kwa michango yao katika sekta mbalimbali nchini Tanzania ikiwemo elimu na pia amewaomba wananchi wa Newala kuutunza mradi huo ili udumu.

Mhe. Rais Magufuli pia amewaeleza wana Newala kuwa Serikali imedhamiria kupambana na dhuluma hasa kwa wakulima wa kipato cha chini kwa kuzuia kangomba na kuamua kununua korosho kwa shilingi 3300 na mpaka sasa asilimia 90 ya wakulima wameshalipwa na waliobaki wanaendelea kulipwa. Amesisitiza kuwa lengo la Serikali la kupeleka fedha moja kwa moja kwa wakulima ni kuboresha maisha yao.

Wakati huohuo Mhe. Rais Magufuli amewasamehe wananchi wote walionunua korosho kwa kangomba na amewaahidi wote walionunua korosho kwa kangomba watalipwa fedha zao kulingana na kiasi cha korosho walichouza kwa masharti ya kuomba msamaha kwa kuandika barua na kuahidi kutorudia tena kununua kangomba.

Pia aliahidi barabara ya kutoka Mtwara mpaka Newala itatengenezwa kwa lami kwa kilomita 100 kuanzia Mnevata hadi Newala na aliwapongeza wana Newala kwa kufanya vizuri katika kilimo na kukuza uchumi wa Wilaya na aliwataka kuendelea kuiamini Serikali na kufanya kazi kwa bidii na maendeleo yatapatikana.

Ziara ya Mhe. Rais Magufuli katika Wilaya ya Newala ilikuwa ya siku moja na aliongozana na viongozi mbalimbali wakiwemo Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe.Pamela O’Donnell, Mawaziri wa wizara mbalimbali, Wabunge, Mkuu wa  Mkoa wa Mtwara, wakuu wa Wilaya na wakurugenzi wa  Halmashauri.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • NEWALA DC YAPOKEA MITUNGI YA GESI

    June 24, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa