• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Kampeni ya kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka mitano yazinduliwa Newala.

Posted on: June 21st, 2021

Kampeni ya kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano ambao hawajapata vyeti vya kuzaliwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Newala imezinduliwa leo tarehe 21/06/2021.

Kampeni hiyo imehusisha mafunzo ya siku moja kwa wasajili ngazi ya kata na vijiji, na usajili na utoaji wa vyeti kwa watoto chini ya miaka mitano kwa siku nne mfululizo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Duncan Thebas, akifungua mafunzo ya wasajili kuelekea kampeni ya usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano. 

Akifungua mafunzo maalum kwa wasajili wa zoezi hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Duncan Thebas amewataka wasajili hao kufanya kazi kwa uadilifu kwa kuwatambua watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano, wanaotakiwa kupata vyeti vya kuzaliwa ili wapate.

"Moja ya ulinzi wa mama na mtoto ni takwimu za mtoto wake mwenyewe, hivyo tukachukue takwimu zote za watoto ambazo zipo katika maeneo yetu." Alisema Ndg. Thebas

Dhumuni kuu la kuanza na mafunzo hayo ni kukumbushana majukumu ya wasajili hao na kujua changamoto wanazokumbana nazo katika kazi hiyo na kutafutia ufumbuzi wa pamoja ili kuleta ufanisi zaidi katika kampeni hiyo.

Mwezeshaji kutoka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) makao makuu Bw. Baraka Mollel, akitoa maelekezo kwa wasajili namna ya kujaza rejista ya taarifa za mtoto anayetakiwa kutengenezewa cheti cha kuzaliwa. 

Akiwezesha mafunzo hayo, Bw. Baraka Mollel kutoka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) makao makuu ameeleza kuwa RITA, UNICEF na Ubalozi wa CANADA walianzisha mfumo wa usajili wa watoto chini ya miaka mitano kwa kuwa kundi hilo la watoto ni muhimu na ni kiashiria muhimu katika mpango wa maendeleo endelevu.

"Katika siku hizi za kampeni, mtoto mwenye umri chini ya miaka mitano anaweza kusajiliwa sehemu yoyote katika ardhi ya Tanzania. Aidha baada ya kampeni hii, watoto wanatakiwa kusajiliwa katika eneo la Halmashauri husika waliyozaliwa na ambao wapo ndani ya siku 90 baada ya kuzaliwa, waliozidi siku 90 watatakiwa kusajiliwa katika ofisi za wakuu wa Wilaya." Alisema Bw. Mollel.

Washiriki wa mafunzo ya usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano wakifuatilia mafunzo ya ujazaji rejesta za taarifa za watoto kwa vitendo.

Kampeni hii ya siku tano inahusisha siku moja ya kikao kazi na siku nne za kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano. 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • NEWALA DC YAPOKEA MITUNGI YA GESI

    June 24, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa