• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Kamati ya ulinzi na usalama wa mwanamke na mtoto yapatiwa mafunzo Newala.

Posted on: June 12th, 2021

Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa mwanamke na mtoto wamepatiwa mafunzo juu ya majukumu yao katika ulinzi na usalama wa mwanamke na mtoto.

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 08/06/2021 yalihusu utekelezaji wa kuimarisha uchumi wa kaya; mila na desturi za jamii; mazingira salama ya mwanamke na mtoto; malezi bora, kuimarisha mahusiano katika kaya na kuziwezesha familia juu ya haki na wajibu wa mtoto; utekelezaji na usimamizi wa sheria za mtoto; huduma kwa waathirika wa ukatili na mazingira salama shuleni na stadi za maisha.

Malengo ya mafunzo hayo ni kuiwezesha kamati ya ulinzi na usalama wa mwanamke na mtoto kutekeleza vyema Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza ukatili dhidi ya wanawakena watoto (MTAKUWA) ambao unalenga kusimamia haki na maendeleo ya mtoto na kuzuia ukatili dhidi ya mwanamke na mtoto na kuhakikisha wanapata haki zao na kutimiza wajibu wao vyema.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Mratibu wa MTAKUWA wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Bakari Mnali, amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana kwa kuwa yanaiwezesha kamati ya MTAKUWA kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

"Mafunzo haya yanawawezesha wajumbe wa kamati ya MTAKUWA kujua majukumu yao na namna watakavyofanya kazi katika swala zima la ulinzi na usalama wa mwanamke na mtoto." Alisema Bw. Mnali.

Akifunga mafunzo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Bi. Lucy Matem ambaye ni Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, amewataka wajumbe hao kutimiza wajibu wao na kuzingatia yale yote waliyofundishwa ili kutimiza adhma ya ulinzi na usalama wa wanawake na watoto. 

Mafunzo hayo yamefanyika kwa siku tano na yaliwahusisha wajumbe wa MTAKUWA wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala wakiwemo wataalam, wawakilishi wa watu wenye ulemavu, wawakilishi wa vikundi vya maendeleo ya wanawake na viongozi wa dini ambao ni wajumbe wa MTAKUWA kulingana na muongozo wake.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa