• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Kamati ya Siasa Wilaya ya Newala yaridhishwa na utekelezaji wa ilani ya CCM Newala

Posted on: February 4th, 2021

Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Newala leo Alhamisi tarehe 4/2/2021 imefanya ziara ya kufuatilia utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwa kutembelea miradi minne ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri.

Kamati hiyo ikiongozwa na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Newala Bw. Jabir Mtanda, imefanikiwa kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Mkwiti-Lochinu-Nyangao ambapo kipande cha urefu wa Km 3.5 kitatengenezwa ili kufungua mawasiliano katika kijiji cha Lochinu na Nyangao.

Akiwasilisha taarifa ya mradi kwa kamati hiyo, mhandisi wa TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Sylvester Balama ameeleza kuwa katika kuhakikisha barabara hiyo inapitika, kwa mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali imetenga jumla ya Tsh.90,864,750.00.

"utengenezaji wa barabara hii utahusisha matengenezo ya kawaida, matengenezo ya sehemu korofi, matengenezo ya muda maalum, ujenzi wa boksi kalavati moja na kalavati la kawaida moja." Alisema mhandisi Balama.

Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Newala ikipokea maelezo ya mradi wa ujenzi wa madarasa mawili na ofisi moja katika shule ya sekondari Mpotola 

Wakiendelea na ziara hiyo, kamati ya siasa ya Wilaya ya Newala pia ilifanikiwa kukagua mradi wa ujenzi wa madarasa mawili na ofisi moja katika shule ya sekondari Mpotola  wenye thamani ya Tsh. 40,000,000 ambao umekamilika; mradi wa usambazaji wa umeme katika kijiji cha Mchemo; na mradi wa ujenzi wa majengo ya maabara na mapokezi ya wagonjwa wa nje (OPD) katika hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Aidha Mhe. Mtanda ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo na kusisitiza fedha zote zinazoletwa na Serikali zitumike vizuri kama ilivyoelekezwa na miradi ikamilike kwa wakati.

"Nimekagua miradi yote minne na nimeridhika kuwa thamani ya fedha na namna miradi inavyotekelezwa vinalingana." Amesema Mhe. Mtanda.

Kamati hiyo ya siasa ya Wilaya ya Newala imefanya ziara hiyo ikiwa ni moja ya shughuli zilizofanywa katika kuadhimisha miaka 44 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA KAZI YA SENSA 2022 July 19, 2022
  • MAELEKEZO KWA WATUMISHI WA AJIRA MPYA ZA WALIMU NA KADA YA AFYA. July 03, 2021
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KITAIFA MKOANI MTWARA KATIKA WILAYA YA NEWALA,HALMASHAURI YA WILAYA NEWALA KATA YA MPWAPWA KIJIJINI MPWAPWA

    September 15, 2022
  • UZINDUZI WA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KITAIFA MKOANI MTWARA KATIKA WILAYA YA NEWALA,HALMASHAURI YA WILAYA NEWALA KATA YA MPWAPWA KIJIJINI MPWAPWA

    September 15, 2022
  • UFUNGUZI WA MAFUNZO YA ULINZI NA USALAMA KWA MWANAMKE NA MTOTO

    December 20, 2021
  • MAFUNZO YA UDHIBITI WA SUMUKUVU KWA MAZAO KILIMO

    December 13, 2021
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa