• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

DC Newala azindua rasmi zoezi la upandaji wa miti kwa wilaya ya Newala

Posted on: February 17th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Newala Bi. Aziza Mangosongo siku ya Ijumaa tarehe 15 Februari 2019 amezindua rasmi zoezi la upandaji wa miti Wilaya ya Newala kwa mwaka huu 2019 katika eneo la shule ya msingi Mtunguru iliyopo kata ya Mtunguru Wilaya ya Newala.

Mkuu wa Wilaya ya Newala Bi. Aziza Mangosongo (aliyesimama) akizungumza na waliohudhuria kwenye uzinduzi wa upandaji wa miti kiwilaya.

Upandaji huo wa miti ni njia ya kutunza mazingira ikiwa ni pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi yanayosababishwa hasa na ukataji wa miti unaopelekea kukosekana kwa mvua za kutosha hivyo kuathiri shughuli za kilimo ambacho ni tegemeo kubwa kwa wananchi wa Newala.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae akishiriki kupanda mti na mwanafunzi wa darasa la awali shule ya msingi Mtunguru

Akizungumza baada ya zoezi la upandaji wa miti hiyo, Afisa Misitu mwandamizi wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Lukumbwiso Mbwilo ameeleza kuwa jumla ya miti 960 imepandwa kwa siku hiyo ambayo inajumuisha miti ya mbao, matunda pamoja na mikorosho. Aidha zoezi hilo ni endelevu katika maeneo yote ya Wilaya ya Newala kwa kuwa Wilaya inatakiwa kupanda miti 1,500,000 na Halmashauri ya Wilaya ya Newala pekee inatakiwa kupanda miti 750,000 katika maeneo yake mbalimbali.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Newala, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae, wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, viongozi wa chama cha mapinduzi CCM, meneja wa benki ya NMB Newala, meneja wa wakala wa misitu Wilaya ya Newala, waheshimiwa madiwani, na wananchi wa kata ya Mtunguru.

Diwani wa kata ya Mtunguru Mhe. Chitwanga Ndembo akishiriki kupanda mti katika eneo la shule ya msingi Mtunguru.

Zoezi la upandaji wa miti ni agizo la Serikali ambapo kila mwaka ni lazima kuwe na siku maalum ya kupanda miti. Kwa mwaka huu 2019 kitaifa zoezi hili litazinduliwa rasmi tarehe 01 Aprili 2019 ila kwa kuwa mwezi Aprili msimu wa mvua kwa Wilaya ya Newala utakuwa unafikia mwisho ndiyo maana uzinduzi kiwilaya umefanyika rasmi mwezi huu Februari.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa