• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Chuo cha VETA kujengwa Kitangari Halmashauri ya Wilaya ya Newala

Posted on: February 18th, 2019

Bodi ya taasisi ya maendeleo Newala NDF leo imekabidhi rasmi shule ya sekondari kitangari NDF kwa Chuo cha mafunzo ya ufundi stadi VETA Tanzania.

Makabidhiano hayo ya majengo na eneo la shule yamefanyika baina ya mwenyekiti wa NDF Mhe. Chitwanga Ndembo na Kaimu Mkurugenzi wa VETA Tanzania Mhandisi Joseph Mwanda na yameshuhudiwa na wajumbe wa bodi ya NDF, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae, mbunge wa Newala mjini Mhe. George Mkuchika, waheshimiwa madiwani, wenyeviti wa serikali za vijiji vya kitangari Hospitali na kitangari sokoni na viongozi wa dini.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, mheshimiwa Ndembo alisema kuwa dhumuni kubwa la kuanzisha chuo hicho cha VETA ni kuwawezesha vijana wa Newala na Tanzania kwa ujumla kupata elimu ya ufundi stadi hivyo kwenda sambamba na kauli mbiu ya Serikali ya kuijenga Tanzania ya Viwanda.

Mwenyekiti wa bodi ya taasisi ya maendeleo Newala Mhe. Chitwanga Ndembo (aliyesimama) akizungumza wakati akikabidhi majengo ya Sekondari ya kitangari NDF kwa VETA Tanzania

Aidha, wanafunzi ambao bado wapo katika shule hiyo wataendelea kusoma katika kipindi hiki cha mwaka mmoja wakati VETA wanakarabati majengo hayo ya shule ili yafanane na mazingira ya chuo cha ufundi stadi na baadaye wanafunzi hao watahamishiwa katika shule nyingine.

Kwa upande wake, kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA Tanzania amesema kuwa ni faraja kubwa sana wao kuanzisha chuo Newala na wameshaleta fedha kiasi cha shilingi milioni mia mbili na ishirini na mbili kwa ajili ya ukarabati wa awali wa majengo hayo na mafunzo yataanza rasmi mwezi wa sita mwaka huu kwa kuanzisha kozi mbili za ufundi.

Kaimu Mkurugenzi wa VETA Tanzania mhandisi Joseph Mwanda (aliyesimama) akieleza matarajio ya VETA Tanzania kwa uanzishaji wa chuo hicho Kitangari, Halmashauri ya  Wilaya ya Newala.

Uanzishwaji wa chuo hicho ni fursa kwa wakazi wa Newala kwa kuwa vijana watapata nafasi ya kusoma, wananchi watakuwa na fursa ya kupata ajira mbalimbali katika chuo hivyo kukuza ujuzi na uchumi wa wananchi wa Newala na Mkoa wa Mtwara kwa ujumla.




Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa