• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Baraza la Madiwani lawafukuza kazi Watumishi 26 wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Posted on: April 29th, 2018

Baraza la madiwani la halmashauri ya Wilaya ya Newala, limewafukuza kazi watumishi 26 wa halmashauri ya Wilaya ya Newala baada ya kuthibitika na makosa mbalimbali ya kiutumishi.

Akithibitisha maamuzi hayo yaliyofanywa katika mkutano wa baraza la madiwani uliofanyika tarehe 29/04/2018 siku ya jumapili, mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Newala Mhe. Rashidi Chitwanga Ndembo amesema baraza limefanya maamuzi hayo baada ya kufanya uchunguzi wa kina na kufuata sheria na taratibu zote za kiutumishi, ambapo watumishi 14 kati yao, walibainika kuwa wameghushi vyeti vya kidato cha nne kwa miaka tofauti tofauti, na wengine 12 walifanya makosa ya utovu wa nidhamu ikiwa ni pamoja na kuidanganya halmashauri na serikali kwa ujumla, hivyo baraza la madiwani limeamua rasmi kuwafukuza kazi watumishi hao 26 wa halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Katika hatua nyingine, kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Newala Mhandisi Nsajigwa P. Sadiki amewasilisha taarifa yake ambapo katika ukaguzi wa hesabu kwa mwaka wa fedha 2016/2017, halmashauri ya wilaya ya Newala imekuwa ni miongoni mwa halmashauri zilizopata HATI SAFI, jambo ambalo limetokana na jitihada na ushirikiano wa waheshimiwa madiwani na watendaji wake katika kuhakikisha halmashauri inafanya shughuli zake kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

Katika taarifa yake Mhandisi Nsajigwa ameongeza kuwa, kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018, halmashauri ya wilaya ya Newala imefanikiwa kununua gari mbili aina ya Toyota Hilux zenye thamani ya Tshs 179,917,273.90 ambapo kila gari limenunuliwa kwa Tshs 89,958,636.95, pamoja na pikipiki mbili  kwaajili ya shughuli za uboreshaji wa ukusanyaji wa mapato na ugani.

Kupitia taarifa hiyo, Mkuu wa wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo, ameipongeza halmashauri ya wilaya ya Newala kwa utendaji mzuri wa kazi na kupata hati safi, huku akisisitiza kuongeza jitihada zaidi katika swala la ukusanyaji wa mapato ya halmashauri.

Ikumbukwe kuwa serikali ya awamu ya tano imekuwa ikipambana vikali na watumishi walioghushi vyeti (vyeti feki), na wale wote wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo, ikiwa ni pamoja na kuwashughulikia watumishi wanaokosa nidhamu ya kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa