• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

NEWALA DC YATEKELEZA MPANGO WA TASAF KWA MAFANIKIO MAKUBWA

Posted on: July 17th, 2025

Na Shabani Mkumba – Afisa Habari, Halmashauri ya Wilaya ya Newala


NEWALA, MTWARA – Julai 16, 2025


Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) unaotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala umeendelea kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi kupitia afua mbalimbali zinazolenga kuinua maisha ya wananchi wa kipato cha chini.


Akitoa taarifa hiyo Julai 16,2025, Mratibu wa TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Ndugu Benjamin Macha, amesema kuwa mpango huo unatekelezwa katika vijiji 107, ukihusisha kaya za walengwa 3,499 zenye wanufaika 10,536, wakiwemo wanawake 6,680 na wanaume 3,856.


Kwa mujibu wa Mratibu huyo, afua zinazotekelezwa kupitia TASAF ni pamoja na uhawilishaji wa fedha, utoaji wa ajira za muda (PWP), uundaji wa vikundi vya kuweka na kukuza uchumi, pamoja na utoaji wa ruzuku za uzalishaji kwa kaya zenye vigezo.


“Kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025, Halmashauri imepokea kiasi cha Shilingi 762,266,964.00 kwa ajili ya uhawilishaji wa fedha. Kati ya fedha hizo, Shilingi 607,822,056.00 ni kwa ajili ya malipo kwa kaya, na Shilingi 154,444,908.00 ni kwa ajili ya shughuli za usimamizi katika ngazi ya Halmashauri na vijiji,” amesema Macha.


Aidha, kupitia miradi ya ajira ya muda (PWP), Halmashauri imetekeleza miradi 116 yenye thamani ya Shilingi 308,050,424.48 kuanzia mwaka 2021 hadi 2025, ambapo walengwa wenye uwezo wa kufanya kazi walipewa ajira za muda huku wakishiriki katika miradi ya kijamii.


Kuhusu uundaji wa vikundi vya kuweka akiba, Ndugu Macha amefafanua kuwa hadi kufikia Juni 2025, Halmashauri imeunda jumla ya vikundi 324 vyenye wanachama 3,524 ambapo wanawake ni 2,725 na wanaume 799. Vikundi hivi vimefanikiwa kujiwekea akiba ya Shilingi 95,030,200.00 na kukopeshana Shilingi 43,681,600.00, ikiwa ni jitihada za kukuza uchumi wa kaya maskini.


Katika hatua nyingine, Halmashauri imewezesha kaya 75 kupokea ruzuku ya uzalishaji baada ya kutimiza vigezo. Kila kaya ilipata mtaji wa Shilingi 350,000.00, ambapo shughuli zilizofadhiliwa ni pamoja na uanzishaji wa biashara ndogondogo, ufugaji, ubanguaji wa korosho na ushonaji wa nguo.


Kwa mujibu wa Mratibu huyo, mafanikio makubwa yamepatikana kupitia utekelezaji wa mpango huo, ikiwa ni pamoja na watoto wote chini ya miaka mitano kuhudhuria kliniki kwa asilimia 100, na wanafunzi kutoka kaya za walengwa kuhudhuria shuleni kwa kiwango sawa.


Hata hivyo, amebainisha changamoto kadhaa zinazokabili utekelezaji wa mpango huo, zikiwemo baadhi ya walengwa kushindwa kuhudhuria siku za malipo, wasimamizi wa ngazi ya jamii (CMC) kujitoa, pamoja na baadhi ya vikundi kuvunjika.


“Tunayo mikakati ya kuimarisha utekelezaji wa mpango huu ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa walengwa, kuimarisha usimamizi wa vikundi, na kuwasaidia kupata mikopo kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ili kuongeza mitaji,” amesema Mratibu Benjamin Macha.


Kwa ujumla, mpango huu umeendelea kuboresha maisha ya wananchi na kuunga mkono juhudi za serikali katika kupunguza umasikini vijijini. Halmashauri ya Wilaya ya Newala inaendelea kusisitiza usimamizi na uwajibikaji katika kila ngazi ili kuhakikisha mafanikio haya yanaimarishwa zaidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • NEWALA DC YATEKELEZA MPANGO WA TASAF KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    July 17, 2025
  • MWEZI WA AFYA NA LISHE KWA WATOTO

    July 04, 2025
  • UJUMBE WA SHUKRANI KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

    July 04, 2025
  • NEWALA DC YAPOKEA MITUNGI YA GESI

    June 24, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa