Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Newala, Bi. Marry Twamgabo, amehimiza ushirikiano na mshikamano kati ya Madiwani, viongozi wa Halmashauri na wataalamu katika kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuongeza ukusanyaji wa mapato na kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati. Amesema juhudi za pamoja ndizo zitakazowezesha Halmashauri kufikia malengo ya maendeleo endelevu na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Akitoa salamu za Mkuu wa Wilaya ya Newala katika Mkutano wa Baraza la Madiwani robo ya pili uliofanyika tarehe 23 Januari 2026, Bi. Twamgabo amewataka Madiwani kuendelea kuhamasisha wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanahudhuria shule kwa wingi, akisisitiza umuhimu wa elimu kwa mustakabali wa wilaya hiyo.
“Elimu ndiyo itakayozalisha wataalamu wa baadaye kutoka Newala. Tukiwahimiza watoto wetu kusoma, tutakuwa tunajenga msingi imara wa maendeleo na wasomi watakaoiinua Wilaya yetu,” alisema Bi. Marry Twamgabo.
Mkutano huo wa Baraza la Madiwani robo ya pili mwaka 2026 uliongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Mhe. Sawanina Jaziri Mohamedi, ambaye alitumia nafasi hiyo kuwaasa wataalamu kuzingatia ushauri unaotolewa na Madiwani kupitia vikao vya kamati za kudumu, ikiwemo kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kuimarisha ukusanyaji wa mapato. Aidha, aliwahimiza Madiwani wenzake kusimamia kwa karibu miradi ya maendeleo katika kata zao ili kuhakikisha matokeo chanya yanapatikana kwa wananchi.
@mtwarars_habari
@msemajimkuuwaserikali
@ortamisemi
@dc_newala
@newalafmtz
Kitangari,Newala
Anuani ya Posta: P.O. Box 16
Simu: +255232410251
Mobile:
Barua pepe: ded@newaladc.go.tz
Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa