Halmashauri ya Wilaya ya Newala imepiga hatua kubwa katika kujitegemea kifedha baada ya kufanikiwa kusajili kampuni yake iitwayo NEWALA BEST BUILDERS AND GENERAL SUPPLY LIMITED COMPANY, ambayo inalenga kuendesha miradi ya ufyatuaji wa tofali na usafirishaji kupitia lori maalum. Kampuni hii imebuniwa ili kuongeza vyanzo vya mapato ya Halmashauri na kupunguza utegemezi wa fedha kutoka serikali kuu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndugu Zefrin Mwenda, wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya pili kilichofanyika tarehe 23 Januari ,2026, miradi hiyo inalenga kusaidia miradi ya ujenzi ndani ya Wilaya kwa bei nafuu na wakati huohuo kuingiza mapato yatakayochochea utekelezaji wa miradi ya maendeleo mingine.
Aidha, Mwenda alieleza kuwa Halmashauri imeanza zoezi la upimaji wa maeneo ya Taasisi zake ikiwemo shule, zahanati, na ofisi za vijiji na kata kwa lengo la kukatia hati miliki. Zoezi hilo ni utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya Bunge, likilenga kulinda mali za umma na kuongeza uhalali wa umiliki wa maeneo hayo.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Newala, Bi Marry Twamgabo, aliipongeza Halmashauri kwa ubunifu wa kuanzisha Kampuni, akisisitiza kuwa kampuni hiyo itakuwa kichocheo cha uchumi wa ndani na chanzo kipya cha mapato. Alitoa wito kwa Madiwani na wataalamu kuongeza ushirikiano na kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi wa Newala DC
@chikaladigitaltv
@ortamisemi
@mtwarars_habari
@msemajimkuuwaserikali
@dc_newala
@newalafmtz
Kitangari,Newala
Anuani ya Posta: P.O. Box 16
Simu: +255232410251
Mobile:
Barua pepe: ded@newaladc.go.tz
Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa