• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Wilaya ya Newala yaadhimisha siku ya sheria nchini

Posted on: February 7th, 2019

Mahakama ya Wilaya ya Newala imeadhimisha siku ya sheria nchini siku ya Jumatano tarehe 06/02/2019 katika viwanja vya mahakama ya Wilaya ya Newala kwa kuwakumbusha wadau wa mahakama  kutimiza wajibu wao kwa kufuata maadili ili wananchi waweze kupata haki zao.

Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo mahakimu wa ngazi mbalimbali wa mahakama ya mwanzo, watumishi wa idara za ofisi za serikali, mashirika ya umma na asasi zisizo za kiserikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa na wananchi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, kwa niaba ya hakimu mkazi wa Wilaya ya Newala, Bi. Devotha Salum amesisitiza kuwa wadau hao ambao ni Polisi, Magereza, Bunge, taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa, wadhamini, ofisi zote za serikali, wazee wa baraza na mawakili wa kujitegemea wanatakiwa kuwa watii wa sheria, waaminifu, wavumilivu na waelewa wa tabia za watu, wanaopenda ukweli na uwazi, na wanaopenda kujifunza na kubadilika ili waweze kutoa huduma na haki kwa wananchi.

Akiendelea kuzungumza na wananchi, Bi.Devotha ameeeleza kuwa wajibu wa mahakama ni kutoa na kusimamia haki kwa kufuata misingi ya sheria na hasa katika dhana nzima ya mgawanyiko wa madaraka na kuwa Mahakama ni lazima iwe huru katika kutoa maamuzi yake bila kuingiliwa na mihimili mingine.

Siku ya sheria nchini huadhimishwa kila mwaka na ni maalum kwa kutoa elimu kwa umma na pia kukumbushana wajibu, kujikosoa na kuwa tayari kukosolewa kwa dhamira moja ya kuwatumikia wananchi ili kuhakikisha haki inapatikana.

Katika maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae alipata nafasi ya kuzungumza ambapo aliwataka wananchi wa Newala kumrudia Mungu na kukemea tabia ya vijana kuwapa ujauzito wanafunzi na kupelekea watoto hao kukatiza masomo yao hivyo kuua ndoto na malengo yao.


'Newala tubadilike, taarifa za mimba kwa wanafunzi ni nyingi. Watoto wana haki ya msingi ya kupata elimu, tuwaache wasome, tuwasimamie kama wazazi. Leo ni siku ya haki hivyo iwe vuguvugu la kuanzisha utoaji wa haki kwa watoto. Sisi ni wadau hivyo tushirikiane kuufichua uovu huu na kutoa ushahidi' alisisitiza Bw. Chimae.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya sheria nchini kwa mwaka 2019 ni 'UTOAJI WA HAKI KWA WAKATI: WAJIBU WA MAHAKAMA NA WADAU'.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa