• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Wanafunzi waaswa kutotumia mwanya wa chanjo ya mlango wa kizazi kuendeleza vitendo vya ngono.

Posted on: April 25th, 2018

Wanafunzi wote wa shule za msingi na sekondari Wilayani Newala, wameaswa kutotumia mwanya wa kupata chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi, kuendeleza vitendo vya ngono, wakiamini kwamba tayari wanayo kinga ya ugonjwa hatari na hivyo wapo huru kutumika watakavyo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo, alipokuwa akizindua rasmi chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi, uzinduzi uliofanyika tarehe 25/04/2018 katika shule ya sekondari Mpotola, iliyopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara.

Mhe. Mangosongo amesema chanjo hiyo inahusisha watoto wakike wenye umri wa miaka 14, ambao kimsingi wengi wao bado ni wanafunzi na ni taifa la kesho, hivyo haina sababu kwa wao kutumia kigezo cha kupata chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi, kiwe ruksa ya kuwa huru kuendeleza tabia mbaya ya kufanya ngono wakiwa masomoni, na hivyo wajiepushe kabisa na vitendo vya ngono, kwani kufanya hivyo kunaweza kuhatarisha maisha yao ya sasa na ya baadae, ikiwa ni pamoja na kukatisha ndoto zao.

Katika uzinduzi huo, Mhe. Mangosongo pia ameishukuru serikali ya awamu ya tano chini ya Wizara ya afya,maendeleo ya jamii jinsia na watoto kwa kuliona hili na kutoa chanjo kwa watoto, na kwa kufanya hivyo, serikali itaokoa maisha ya ya watanzania wengi, kwani utafiti unaonyesha zaidi ya 30% ya vifo vitokanavyo na saratani kwa wanawake, vinasababishwa na saratani ya mlango wa kizazi, ikifuatiwa na saratani ya matiti.

Aidha lengo la serikali kuanzisha chanjo hii, ni kupunguza vifo vitokanavyo na saratani, kupunguza gharama za matibabu kwani inakisiwa kuwa kumtibu mgonjwa mmoja mwenye saratani,ni shilingi milioni 5.5 ukiacha gharama nyingine za uchunguzi, wakati kupata chanjo moja itakayomkinga mtu na saratani ya mlango wa kizazi ni shilingi elfu 30 tu.

Katika hafla hiyo ya uzinduzi wa chanjo iliyoambatana na siku ya malaria Duniani, halmashauri ya Wilaya ya Newala kupitia idara ya afya, imefanya zoezi la upimaji wa ugonjwa wa malaria, ambapo jumla ya watu 198 waliokuwepo kwenye hafla hiyo waliweza kupimwa malaria, na 61 kati yao, vipimo vimeonyesha kuwa wana  na ugonjwa wa malaria na hivyo wamepatiwa dawa za kutibu malaria, na wakati huo huo pia watu 24 wameweza kupewa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi, watoto 8 wamepata chanjo ya polio ya matone matatu, watoto 8 pia wamepata chanjo ya polio sindano na mtoto mmoja tu amepata chanjo ya polio matone ama polio zero kwa lugha ya kitaalamu.

Kauli mbiu ya siku ya malaria Duniani mwaka huu wa 2018 ni

“Mimi nipo tayari kutokomeza malaria Tanzania, wewe je?”

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa