• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Uzinduzi wa Upandaji wa miti Mkoa wa Mtwara wafanyika Newala.

Posted on: February 13th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa jana tarehe 12/02/2021 amezindua zoezi la upandaji wa miti kwa Mkoa wa Mtwara katika eneo la shule ya sekondari Mpelepele iliyopo katika kijiji cha Mdimba Mpelepele Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo akizungumza katika uzinduzi wa upandaji wa miti kwa Mkoa wa Mtwara katika shule ya sekondari Mpelepele 

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhe. Mangosongo kuwa upandaji wa miti katika maeneo yetu una faida kubwa.

"miti ni chanzo cha chakula, ni malighafi pia ni chanzo cha hewa safi. Nitumie fursa hii kuwataka wa Mtwara kupanda miti na kuitunza." alisema Mhe. Mangosongo.

Mhe. Mangosongo pia ametoa wito kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Mtwara kuandaa programu za kupanda miti na kuitunza, kuongeza bajeti ya mazingira kwa kuandaa vitalu vya miche ya miti na kuigawa bure kwa wananchi na kudhibiti uchomaji moto wa mashamba kwa kuweka sheria ndogo za Halmashauri zinazozuia vitendo hivyo.

"Mkoa wa Mtwara unaendelea kusimamia sheria ya misitu namba 14 ya mwaka 2002 na kanuni zake kwa lengo la kuhakikisha kuwa uharibifu wa misitu unaosababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile uvunaji haramu wa misitu, kilimo cha kuhamahama, upanuzi holela wa mashamba ya kilimo, ufugaji holela wa mifugo na uchomaji wa misitu unakomeshwa." Alisema Mhe. Mangosongo.

Akiendelea na uzinduzi huo, Mhe. Mangosongo pia amewaeleza wananchi kuwa sekta hii ni muhimu sana katika ukuaji wa uchumi hasa ukizingatia Taifa lipo katika uchumi wa kati na linatekeleza mkakati wa uchumi wa viwanda.

"Serikali chini ya uongozi wa Mhe. Dokta John Pombe Magufuli imeweka kipaumbele katika swala la kuhifadhi rasilimali za misitu na ufugaji wa nyuki ili sekta hiyo izalishe ajira nyingi zaidi kupitia mazao yake." Alisema Mhe. Mangosongo.

Zoezi hilo la uzinduzi wa upandaji wa miti kwa Mkoa wa Mtwara limehusisha upandaji wa miti 1000 ya mbao na matunda katika eneo la shule ya sekondari Mpelepele na ugawaji wa miche 500 kwa wananchi ili wakapande katika maeneo yao.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA KAZI YA SENSA 2022 July 19, 2022
  • MAELEKEZO KWA WATUMISHI WA AJIRA MPYA ZA WALIMU NA KADA YA AFYA. July 03, 2021
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KITAIFA MKOANI MTWARA KATIKA WILAYA YA NEWALA,HALMASHAURI YA WILAYA NEWALA KATA YA MPWAPWA KIJIJINI MPWAPWA

    September 15, 2022
  • UZINDUZI WA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KITAIFA MKOANI MTWARA KATIKA WILAYA YA NEWALA,HALMASHAURI YA WILAYA NEWALA KATA YA MPWAPWA KIJIJINI MPWAPWA

    September 15, 2022
  • UFUNGUZI WA MAFUNZO YA ULINZI NA USALAMA KWA MWANAMKE NA MTOTO

    December 20, 2021
  • MAFUNZO YA UDHIBITI WA SUMUKUVU KWA MAZAO KILIMO

    December 13, 2021
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa