• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Uhakiki wa kaya zilizopo kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini unafanyika Newala

Posted on: August 4th, 2020

Timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Newala pamoja na wawezeshaji 23 jana siku ya Jumatatu tarehe 03/08/2020 wamepatiwa mafunzo elekezi juu ya zoezi la uhakiki wa kaya zilizopo kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini unaosimamiwa na TASAF.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bi. Magreth Likonda akifungua mafunzo elekezi ya uhakiki wa walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini.

Akifungua mafunzo hayo elekezi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bi. Magreth Likonda amewataka wawezeshaji hao kufuatilia vizuri na kuelewa mafunzo hayo wanayopewa kwa siku mbili na kufanya vizuri kazi hiyo ya uhakiki ambayo kwa sasa taarifa zake zitajazwa moja kwa moja kwenye mfumo wa TASAF na wawezeshaji hao kwa njia ya simu walizopatiwa maalum kwa zoezi hilo.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji TASAF ambaye pia ni mwezeshaji wa mafunzo hayo Bw. Steven Samwel akitoa mafunzo kwa washiriki katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Akitoa ufafanuzi kwenye mafunzo hayo, mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Steven Samwel, amewaeleza washiriki kuwa uhakiki huo utafanyika katika kaya zote za walengwa kwenye kila kijiji ambacho kipo katika mpango wa kunusuru kaya masikini kwa lengo la kupata orodha halisi ya kaya za walengwa wenye vigezo vya kubaki kwenye mpango.

"Uhakiki huu utafanyika kwa njia ya ukaguzi wa vitambulisho vya walengwa vya mpango, vitambulisho vya Taifa na kukusanya taarifa zote za wanakaya walengwa kwa njia ya kielektroniki. " Alisema Bw. Samwel.

Kwa Wilaya ya Newala, uhakiki huo utafanyika katika vijiji 97 vilivyopo kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini. Aidha zoezi hili la uhakiki ni hatua ya awali ya kuelekea zoezi la uibuaji wa kaya masikini nyingine ambazo zitaungana na kaya zilizohakikiwa na kukidhi vigezo kupokea ruzuku kutoka TASAF katika kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF (PSSN II) ambacho kinatarajiwa kufanya utekelezaji wake kwa kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2020 hadi 2023.

Uhakiki wa kaya hizo ambazo tayari zipo kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini kwa Wilaya ya Newala unatarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia Jumatano tarehe 05/08/2020 hadi Ijumaa tarehe 07/08/2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Utekezaji wa Ujenzi mpya ya Sekondari Mtunguru

    May 29, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA

    May 29, 2025
  • UTEKEZAJI WA ILANI YA CCM

    May 27, 2025
  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa