• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

TAMISEMI yapongeza upanuzi wa kituo cha afya Kitangari

Posted on: June 7th, 2018

Ofisi ya Rais – Tamisemi imeipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwa hatua nzuri iliyofikia ya upanuzi wa kituo cha Afya Kitangari na kusema kuwa ujenzi wa miundombinu ya kituo hicho ni mfano wa kuigwa na Halmshauri nyingine hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu – TAMISEMI upande wa Afya Dkt Zainabu Chaula alipokuwa katika ziara yake ya kikazi iliyofanyika tar 6/6/2018 Wilayani Newala, ambapo alitembelea mradi wa upanuzi wa miundombinu ya kituo cha Afya Kitangari, ambao kwa sasa upo katika hatua ya umaliziaji.

Dkt Chaula amesema wameridhishwa na kufurahishwa na usimamizi mzuri wa mradi huo na kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae kwa kuhakikisha fedha za wananchi pamoja na serikali zinatumika ipasavyo katika kuboresha huduma za Afya na uzazi salama, na kwamba katika maeneo mbalimbali waliyopita Mkoani Mtwara, Mradi wa kituo cha Afya Kitangari umeonyesha sura ya kipekee inayovutia na inayopaswa kuigwa na Halmashauri nyingine.

Pamoja na kuridhishwa na hali nzuri ya majengo yaliyojengwa katika kituo hicho, pia yapo baadhi ya maeneo machache ambayo Naibu Katibu Mkuu – Tamisemi na kamati yake, wametoa ushauri wa kuyaboresha zaidi na kuongeza baadhi ya vitu, ili kukidhi haja ya upatikanaji huduma pindi huduma hiyo itakapozinduliwa, kwani lengo la serikali ni kuja kuzindua huduma na sio majengo.

Kutokana na hatua nzuri ya upanuzi wa kituo hicho cha Afya Kitangari, Naibu Katibu Mkuu – Tamisemi amesema kuwa serikali ipo tayari kuleta watumishi wa idara ya Afya watakaofanya kazi ya utoaji huduma kwa wananchi watakaofika kutaka huduma katika kituo hicho cha Afya Kitangari na kwamba watumishi hao watafika pindi tu mradi huo utakapokamilika tayari kwa kuanza kutoa huduma.

Nae Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Dkt Dorothy Gwajima, amewapongeza wananchi wa Kitangari kwa kushirikiana kikamilifu na serikali katika kujitolea kuchangia na kuhakikisha miundombinu bora ya Tiba katika kituo hicho, ikiwa ni pamoja na kuwasisitiza wananchi kuendelea kumiliki huduma zitakapoanza, kwani ipo kamati ya usimamizi wa huduma inayoshirikisha wananchi wa Kitangari, ambayo kimsingi ni sera ya serikali inayowataka wananchi kusimamia kikamilifu mipango na huduma inayotolewa, ikiwa ni pamoja na kumshauri Mkurugenzi kwa niaba ya wananchi juu ya utoaji wa huduma ya Afya katika kituo hicho.  “Sera imewatengenezea mkakati wa kutengeneza hizi kamati za usimamizi maana ni kituo chenu”Alisisitiza zaidi Dkt Gwajima.

Naibu katibu Mkuu - Tamisemi Dkt Zainabu Chaula (wa katikati) Mkurugenzi wa USAID mradi wa Boresha Afya Dkt Marina Njelekela (wa pili kutoka kushoto), Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae, pamoja na viongozi wengine walipokuwa wakiongea na wananchi wa Kitangari, mwishoni mwa Ziara ya ukaguzi wa mradi wa kituo cha afya Kitangari, tarehe 6/6/2018.

Ziara ya Naibu Katibu Mkuu – Tamisemi iliyohusu ukaguzi wa mradi wa kituo cha Afya Kitangari unaogharimu jumla ya shilingi milioni 400, iliwahusisha wageni mbalimbali kutoka Tamisemi na Wizara ya Afya, mganga mkuu wa Mkoa wa Mtwara (RMO),Mkurugenzi wa USAID – Boresha Afya Dkt Marina Njelekela, pamoja na viongozi mbalimbali wa sekta na mashirika yanayotoa misaada ya tiba nchini Tanzania.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA KAZI YA SENSA 2022 July 19, 2022
  • MAELEKEZO KWA WATUMISHI WA AJIRA MPYA ZA WALIMU NA KADA YA AFYA. July 03, 2021
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KITAIFA MKOANI MTWARA KATIKA WILAYA YA NEWALA,HALMASHAURI YA WILAYA NEWALA KATA YA MPWAPWA KIJIJINI MPWAPWA

    September 15, 2022
  • UZINDUZI WA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KITAIFA MKOANI MTWARA KATIKA WILAYA YA NEWALA,HALMASHAURI YA WILAYA NEWALA KATA YA MPWAPWA KIJIJINI MPWAPWA

    September 15, 2022
  • UFUNGUZI WA MAFUNZO YA ULINZI NA USALAMA KWA MWANAMKE NA MTOTO

    December 20, 2021
  • MAFUNZO YA UDHIBITI WA SUMUKUVU KWA MAZAO KILIMO

    December 13, 2021
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa