• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara aiomba mamlaka ya elimu kutoa uhuru wa kubuni ramani ya nyumba za walimu.

Posted on: April 20th, 2018

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe: Gelasias Byakanwa ameiomba mamlaka ya elimu Tanzania kutoa uhuru wa kubuni ramani ya nyumba za walimu pale wanapotoa msaada wa miradi hiyo.

Mhe Byakanwa ameyasema hayo Wilayani Newala, alipokuwa kwenye ziara yake ya kawaida ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika halmashauri ya Wilaya ya Newala siku ya alhamisi tarehe 19/04/2018, ambapo ameshuhudia ujenzi wa nyumba moja ya kaya sita yaani ( six in one) katika shule ya sekondari Lengo iliyopo Wilaya ya Newala, ambao ulianza tangu mwezi wa pili mwaka huu wa 2018, unaofadhiliwa na mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA),  na una gharimu jumla ya shilingi milioni 141 ambazo zimetolewa kwa awamu mbili tofauti, awamu ya kwanza ni shilingi milioni 70.5 na awamu ya pili pia ilikuja milioni 70.5 ambazo jumla yake ni milioni 141 zinazotarajiwa kukamilisha nyumba hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara

Pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasias Byakanwa (wa kwanza kushoto),Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo ( wa pili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae (wa tatu kutoka kushoto) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Mhe. Chitwanga R. Ndembo (anaefuata baada ya Mkurugenzi),wakiwa kwenye mradi wa nyumba ya walimu shule ya sekondari Lengo Wilayani Newala.

Akitoa maoni yake juu ya mradi huo, Mhe Byakanwa amesema mradi wa nyumba inayojengwa katika sekondari hiyo, haitampa uhuru mwanakaya kujitawala na familia yake kulingana na uhalisia  wa maisha halisi ya mtanzania, na hivyo Wizara ya Elimu na mamlaka ambazo zinatoa misaada ya nyumba hizo, zitoe na uhuru kwa taasisi husika kudizaini ramani ya nyumba hizo kulingana na mazingira halisi ya eneo husika na familia za walimu hao, kwani kuwepo kwa nyumba hiyo kunatarajiwa kuleta ufanisi mkubwa kwa walimu na wanafunzi wa shule ya sekondari Lengo.

Katika ziara yake Mhe; Byakanwa pia amekagua mradi wa upanuzi wa miundombinu majengo ya kituo cha afya Kitangali, ambapo amewaomba wananchi wa Kitangali kwa kushirikiana na Diwani wao wa kata ya Kitangali, kujitolea kushiriki kujenga wodi ya kina mama au wodi mchanganyiko ambayo itahusisha wagonjwa wa aina zote, kwani kama wananchi hawatashirikishwa kikamilifu na kujitolea kusaidia ujenzi wa miradi kama hiyo, bado itakuwa vigumu kwa serikali kufanya kila kitu na hivyo kuchelewesha huduma na maendeleo kwa ujumla.

Mradi wa upanuzi wa miundombinu majengo ya kituo hicho cha Afya Kitangali unaogharimu jumla ya shilingi milioni 400, unahusisha ujenzi wa nyumba moja ya mtumishi wa kituo hicho na kuboresha huduma za upasuaji, maabara na huduma ya damu salama, chumba cha kuhifadhia maiti, wodi ya wazazi na watoto, kichomea taka, ikiwa ni pamoja na kupunguza vifo na rufaa za kina mama wajawazito ambao walikuwa wanalazimika kukimbizwa hospitali ya mji Newala.

Aidha Mhe Byakanwa ameziomba taasisi zinazotoa misaada ya miradi hiyo, kutoa mgawanyo wa fedha hizo kulingana na eneo husika kwani maeneo kama ya Newala na Mtwara kwa ujumla kuna changamoto ya mabadiliko ya kupanda kwa bei ya vifaa vya ujenzi mara kwa mara, kama saruji na nondo, ikiwa ni pamoja na upatikanaji mgumu wa rasilimali madini kama mchanga, kokoto na mawe, ambavyo vinaongeza ugumu katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Mradi wa  kituo cha afya Kitangali ulioanza januari 2018, pamoja na mradi wa ujenzi wa nyumba ya walimu wa shule ya sekondari Lengo, inatarajiwa kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu wa 2018.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa