• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

MILIONI 170.5 ZA MFUKO WA JIMBO NEWALA ZACHOCHEA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA

Posted on: July 10th, 2024

NEWALA, MTWARA

Mbunge wa Jimbo la Newala vijijini Mhe. Maimuna Mtanda amesema kuwa Halmashauri ya wilaya ya Newala imepokea fedha shilingi Milioni 170.5 za mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuchochea miradi ya maendeleo katika Jimbo la Newala Vijijini.

   Mhe Mtanda amesema hayo kwa nyakati tofauti wakati akiwasilisha kitabu alichokiandika cha ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025  kwa  Wajumbe wa Mkutano mkuu wa Jimbo wa Tarafa ya Chilangala na Kitangari Julai 9,2014  ambacho kinaelezea utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo zilifanywa na Serikali na Mbunge Mtanda kwa wananchi wa Jimbo la Newala vijijini.

  Amesema kwa Mwaka wa fedha 2021/2022 shilingi Milioni 41.5 zilipokelewa, Mwaka 2022/2023 Milioni 64.5 zimepokelewa na Mwaka 2023/2024 shilingi Milioni 64.5 zimepokelewa na fedha zote zimetumika kwa malengo yaliyokusudiwa kwa  kupeleka fedha na vifaa kama vile saruji na bati kwenye miradi ya vijiji vya kata zote za Newala vijijini.

 " Hapa naomba nitoe ufafanuzi wa fedha za mfuko wa jimbo, kwanza hairuhusiwi kutumia fedha hizi kwa shughuli za kisiasa na shughuli za kidini"

 " Pia fedha za mfuko wa jimbo hutolewa mara moja Kwa mwaka na kupelekwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri na mgao wa fedha hizo hufanywa na Kamati ya mfuko iliyoundwa kwa majibu wa Sheria" amesema Mtanda

Aidha amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha hizo kwani zimesaidia kuchochea maendeleo Jimbo la Newala vijijini.

  Mfuko wa kuchochea maendeleo ya Jimbo ulianzishwa mwaka 2009 kwa Sheria NA. 16 ya Mwaka 2009 ili kusaidia kuchochea maendeleo kwenye majimbo kwa kutekeleza miradi midogo midogo iliyoibuliwa na Wananchi kwenye Vijiji na Kata.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa