• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Mafunzo ukusanyaji takwimu za mradi wa maji na usafi wa mazingira yafanyika Newala

Posted on: July 23rd, 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Newala leo tarehe 23/07/2020 imetoa mafunzo ya ukusanyaji wa takwimu za maji na usafi wa mazingira ngazi ya kaya kwa watendaji wa kata, watendaji wa vijiji na watoa huduma za afya wa kujitolea ngazi ya jamii (WAJA).

Mafunzo hayo ni maandalizi ya utekelezaji wa mradi wa maji (unawaji wa maji tiririka na sabuni) na usafi wa mazingira (utumiaji wa vyoo bora) katika kaya na vituo vya kutolea huduma ya afya unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Bw. Famili Mshaghira akifungua mafunzo ya ukusanyaji takwimu za mradi wa maji na usafi wa mazingira leo tarehe 23/07/2020 katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha walimu Kitangari. 

Akifungua mafunzo hayo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Famili Mshaghira amewataka washiriki wote kutekeleza majukumu yao kwa ufasaha.

"Mradi huu ni wa tunapewa pesa kulingana na matokeo tutakayoyapata katika utekelezaji (P4R), hivyo tunatakiwa kuwa makini katika kutekeleza majukumu yetu ili kuleta mafanikio zaidi katika Halmashauri yetu." Alisema Bw. Mshaghira.

Mafunzo hayo yalihusisha kuwapa washiriki uelewa wa pamoja juu ya mradi wa usambazaji wa maji na usafi wa mazingira vijijini, mapokezi na matumizi ya fedha za mradi, viashiria vya matokeo ya mradi ngazi ya kaya na vituo vya kutolea huduma ya afya, ujazaji wa takwimu za maji safi na usafi wa mazingira na utambuzi wa aina za vyoo na sifa zake.

Aidha mpaka sasa Halmashauri ya Wilaya ya Newala imepokea kiasi cha Tsh. 272,830,000 ambapo Tsh. 220,000,000 zitaenda kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya vya Kitangari, Mkwedu, Chihangu, zahanati za Mpirani, Maputi, Makukwe, Lengo, Mnali, Mnyeu na Mnyambe na zitatumika kujenga vyoo bora vya wagonjwa na watumishi; kuweka mifumo ya maji tiririka/bomba; kuweka sehemu za kunawia mikono katika maeneo yote muhimu na kuweka bafu katika wodi ya wazazi. Pia Tsh.52,830,000 ni kwa ajili ya shughuli za usimamizi na uboreshaji wa huduma za usafi wa mazingira katika kaya.

Mafunzo hayo yatafanyika kwa siku mbili, siku ya kwanza yatahusisha washiriki kutoka kata 9 na siku ya pili kata 13 watakaowezeshwa kukusanya takwimu za usafi wa mazingira za vijiji vyote, shule na vituo vya kutolea huduma ya afya kwa wakati na kwa usahihi zikiwemo utumiaji wa vyoo bora.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Utekezaji wa Ujenzi mpya ya Sekondari Mtunguru

    May 29, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA

    May 29, 2025
  • UTEKEZAJI WA ILANI YA CCM

    May 27, 2025
  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa