• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Newala wachagua mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo

Posted on: December 5th, 2020

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala jana siku ya Ijumaa tarehe 04/12/2020 wamepiga kura ya kumchagua Mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa Halmashauri yao katika mkutano wa baraza la madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha walimu Kitangari.

Mkutano huo wa baraza la madiwani ulianza kwa madiwani wateule wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala kula kiapo mbele ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Nasra Mkadam Mwinshehe; waheshimiwa madiwani kutoa tamko la maadili mbele ya Afisa Maadili kutoka Sekretariet ya Maadili ya viongozi wa umma kanda ya kusini Mtwara, Bi. Esther Lemther Laizer ili madiwani hao wawe waadilifu katika kuwatumikia wananchi kama walivyoapa.

Diwani mteule wa kata ya Mtunguru, Mhe. Chitwanga Ndembo akila kiapo wakati wa Mkutano wa baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Newala. 

Baada ya viapo hivyo, waheshimiwa madiwani walipata nafasi ya kupiga kura ya kumchagua Mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala ambapo Mhe. Ladda Mfaume Tamimu, diwani wa kata ya Kitangari (CCM) alichaguliwa kuwa mwenyekiti na Mhe. Isabela Dadi Makumbuli, diwani wa kata ya Maputi (CCM) kuwa makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwa kura zote za ndiyo kutoka kwa waheshimiwa madiwani 30.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Mhe. Ladda Mfaume Tamimu, akiwashukuru waheshimiwa madiwani kwa kumchagua kuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala. 

"Nawashukuru waheshimiwa madiwani wote kwa kuniamini na kunichagua kuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Mungu awabariki na tuendelee kushirikiana kuijenga Halmashauri yetu." Alisema Mhe. Lada.

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Mhe. Isabella Dadi Makumbuli akiwashukuru waheshimiwa madiwani kwa kumchagua kuwa makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

"Asanteni kwa kunichagua kuwa makamu mwenyekiti, kikubwa tukafanye kazi kwa ushirikiano tukiamini umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Asanteni sana." Alisema Mhe. Makumbuli.

Aidha pia waheshimiwa madiwani walipata nafasi ya kuunda kamati za kudumu za Halmashauri ya Wilaya ya Newala ambapo zilipatikana kamati nne ambazo tano ambazo ni Kamati ya Elimu, Afya na Maji; Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira; Kamati ya Maadili, Kamati ya Ukimwi; na Kamati ya Fedha.

Baraza hilo la madiwani pia lilipata nafasi ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi, shughuli na maamuzi yaliyofanyika katika kipindi cha mwezi Julai hadi Novemba 2020 katika idara mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Mkutano huo wa baraza la madiwani umefanyika kwa siku moja na ulihudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Duncan Thebas, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw. Alphayo Kidata, Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo, wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Newala, Mhe. Mbunge wa jimbo la Newala vijijini Bi. Maimuna Mtanda, viongozi wa vyama vya siasa vya CCM na ACT wazalendo wilaya ya Newala, viongozi wa dini,maafisa wa Maadili Sekretariet ya Maadili ya viongozi wa umma kanda ya Kusini, Hakimu Mkazi wa wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Nasra Mkadam Mwinshehe, waheshimiwa madiwani, wakuu wa idara na vitengo, wageni waalikwa na waandishi wa habari. 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa