• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Kikundi cha bodaboda chakabidhiwa mkopo wa pikipiki 10 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Posted on: May 7th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo leo Ijumaa tarehe 07/10/2021 amekabidhi pikipiki 10 kwa vijana wa kikundi cha bodaboda Kitangari Hospitali waliopatiwa pikipiki hizo na Halmashauri ya Wilaya ya Newala ikiwa na mkopo uliotokana na asilimia kumi ya makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Mmoja wa wanakikundi cha bodaboda cha Kitangari Hospitali akikabidhiwa ufunguo pamoja na kadi ya pikipiki na Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo.

"Kila mwaka wa fedha, Halmashauri ya Wilaya ya Newala huwa inatenga asilimia kumi ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kusaidia makundi maalum ya wanawake, vijana na walemavu kwa kutoa mikopo kwa uwiano wa asilimia 4 kwa wanawake, asilimia 4 kwa vijana na asilimia 2 kwa watu wenye walemavu." Alisema Bw. Ally Said, Kaimu Afisa Maendeleo ya jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

"Kwa mwaka wa fedha 2020/2021, mpaka kufikia mwezi Machi 2021, jumla ya Tsh. 76,764,357 zimetolewa kusaidia vikundi hivyo vya wajasiriamali hao kwa uwiano wa asilimia 4, 4, 2 kikiwemo kikundi hiki cha bodaboda kilichopata pikipiki 10 zilizogharimu Tsh. 22,500,000 ambapo pikipiki nane ni aina ya Sinoray, moja Haujue na moja TVS." Alisema Bw. Said.

Kwa sasa Halmashauri ya Wilaya ya Newala inaelekeza nguvu kubwa kwenye kutoa mikopo ya vifaa vitakavyowafanya wanakikundi kuwekeza kwenye utendaji zaidi.

Akikabidhi pikipiki hizo, Mhe. Mangosongo amewataka wanakikundi hao wanaopatiwa pikipiki kuziendesha kwa kufuata sheria za barabarani, na kuhakikisha wanarejesha fedha hizo kwa wakati ili ziingie kwenye mzunguko wa ukopeshaji wa vikundi vingine. Kila aliyepokea pikipiki alizawadiwa na Mhe. Mangosongo lita mbili za petroli kwa ajili ya kuanzia shughuli zao za biashara ya kubeba abiria.

"Nampongeza Mkurugenzi Mtendaji kwa kutenga fedha hizi na kuwakopesha vijana hawa. Umetekeleza Ilani na agizo la Serikali. Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi inasema tuwajali vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kwa kuwapa mikopo itakayowasaidia kuwapandisha kiuchumi. Hongereni sana. " alisema Mhe. Mangosongo.

Akizungumza kwa niaba ya wanakikundi cha bodaboda cha Kitangari Hospitali, Bw. Said Shaban Athumani, katibu wa kikundi hicho aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwa kuwapatia mikopo hiyo na kuahidi kuwasilisha marejesho ya mkopo wao kwa wakati.

Utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu upo kisheria na Halmashauri ya Wilaya ya Newala mpaka mwezi Machi, 2021 ilitenga Tsh. 79,423,471.74 kwa ajili ya mikopo hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • NEWALA DC YAPOKEA MITUNGI YA GESI

    June 24, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa