• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Halmashauri ya Wilaya ya Newala yapongezwa kwa kupata hati safi ya ukaguzi

Posted on: June 3rd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa jana tarehe 2/6/2020 ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu za mwaka 2018/2019.

Pongezi hizo zimetolewa na Mhe. Byakanwa kwenye baraza maalum la madiwani la kupokea na kujadili taarifa ya Mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali.

Katika ukaguzi huo wa hesabu za kuanzia mwezi Julai 2018 hadi mwezi Juni 2019, Halmashauri ya Wilaya ya Newala ilikuwa na jumla ya hoja 27, kati ya hizo hoja 13 zilipatiwa majibu na kufungwa, hoja 3 zilihamishiwa mamlaka ya maji vijijini (RUWASA) na hoja 11 sawa na asilimia 41 ya hoja zote zinaendelea kufanyiwa kazi.

Wakati huo huo Mhe. Byakanwa ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Newala kuongeza ubunifu kwa vyanzo vipya vya mapato ili iweze kujiendesha na kulipa madeni waliyonayo yakiwemo malipo ya waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Pia katika baraza hilo maalum, Mhe. Byakanwa alitoa tuzo ya Rais ya kuhifadhi mazingira kwa washindi watano waliopatikana kwa kuongoza kutunza na kuhifadhi mazingira vizuri katika maeneo yao.

Mhe. Byakanwa akikabidhi hati ya pongezi kwa washindi wa kwanza wa tuzo ya Rais ya kuhifadhi mazingira ambao ni shule ya sekondari Mmulunga. Waliopokea tuzo hiyo kutoka kulia ni mwalimu mkuu wa shule hiyo, Mhe. diwani wa kata ya Chiwonga na mtendaji wa kata ya Chiwonga

Washindi hao ni shule ya sekondari Mmulunga, shule ya sekondari Mkoma II, kikundi cha uhifadhi wa mazingira cha Umoja kilichopo kwenye kijiji cha Chiwonga, Kijiji cha Mitema pamoja na shule ya msingi Mtunguru ambao wote kwa pamoja wakipewa hati ya pongezi pamoja na fedha taslimu.

Baraza hilo maalum la madiwani lilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha walimu Kitangari.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • NEWALA DC YAPOKEA MITUNGI YA GESI

    June 24, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa