• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Halmashauri ya Wilaya ya Newala yaadhimisha wiki ya unyonyeshaji

Posted on: August 7th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Newala imefanya maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji wa mtoto siku ya Jumanne tarehe 06/08/2019 katika kijiji cha Tuyangatane, kata ya Malatu kwa kuwakumbusha wakazi wa Newala faida za unyonyeshaji.

Akihutubia katika maadhimisho hayo mgeni rasmi ambaye ni kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bi. Magreth Lokonda aliwashukuru shirika la Hellen Keller International kwa kufanikisha maadhimisho hayo, pia alitumia nafasi hiyo kusisitiza umuhimu wa mama aliyejifungua kuanza kumnyonyesha mtoto ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa.

Bi. Likonda alieleza kuwa unyonyeshaji wa mtoto ni muhimu kwa kuwa maziwa ya mama yanamsaidia mtoto kukua vizuri kimwili na kiakili, kumkinga na magonjwa hasa yale ya mfumo wa hewa, mama kupunguza uzito uliopatikana kipindi cha ujauzito na pia unyonyeshaji hutumika kama njia ya asili ya uzazi wa mpango..

Aidha, baba wa watoto na wana familia kwa ujumla wamehimizwa kumsaidia mama kufanya shughuli za nyumbani ili mama apate muda wa kula vizuri, kupumzika na kumnyonyesha mtoto kwa wakati.

Wakati huo huo, Mratibu wa mradi wa Amka kutoka shirika la Hellen Keller International Bw. Juma Mziwanda alieleza kuwa mradi huo wa Amka ‘rise for nutrition’ umewasaidia wakina mama kupata elimu hivyo kuwa na muamko mkubwa wakuwapatia watoto maziwa ya mama tu miezi sita ya mwanzo baada ya kuzaliwa na hivyo kupelekea afya za watoto kuwa nzuri na maradhi ya watoto chini ya miezi sita kupungua. Bw. Mziwanda alisisitiza kuwa mafanikio ya mtoto kimwili na kiakili yanajengwa ndani ya siku 1000 tangu kutungwa kwa mimba.

Aidha, Mratibu wa lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bi. Somoe Bakari alieleza kuwa malengo ya maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji duniani kwa mwaka 2019 ni kuinua uelewa wa jamii kuhusu namna usawa wa kijinsia, sheria na kanuni zinavyoweza kulinda, kuendeleza na kusaidia unyonyeshaji maziwa ya mama na hivyo kuboresha lishe ya watoto.

Maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji kwa watoto kitaifa na kimataifa hufanyika kuanzia tarehe 1 mpaka 7 ya mwezi wa nane kila mwaka. Na kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu 2019 ni ‘Wawezeshe wazazi kufanikisha unyonyeshaji’

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa