• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

DC Newala akabidhi pikipiki kwa Maafisa Elimu Kata.

Posted on: September 13th, 2018

Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo ( wa pili kutoka kushoto) pamoja na viongozi wengine wa Wilaya alipokata utepe kuashiria ufunguzi wa pikipik tayari kwa kukabidhi pikipiki hizo 22 kwa Maafisa Elimu Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala tarehe 13/09/2018.


Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo amekabidhi jumla ya pikipiki 22 kwa Maafisa elimu Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Katika hafla hiyo fupi iliyofanyika leo tarehe 13/09/2018 katika ofisi kuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Mhe. Mangosongo amesema Serikali imeamua kuwapatia Maafisa Elimu kata pikipiki hizo, ili kurahisisha utendaji wa kazi, kufika maeneo ya kazi kirahisi, pamoja na kusimamia swala zima la utoro shuleni kwa watoto, na kuhakikisha walimu nao wanafanya kazi yao ipasavyo.

Wakati wa kukabidhi pikipiki hizo, Mhe. Mangosongo amewaasa maafisa elimu kata hao kuzitumia pikipiki hizo kwa malengo yaliyokusudiwa na Serikali, na si vinginevyo ili kuleta tija katika swala zima la utoaji elimu bure linaloendelea kutekelezwa na Serikala ya awamu ya tano.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa, ametumia fursa hiyo kuwaagiza maafisa Elimu kata kuhakikisha wanasimamia shule zao vizuri, ili kuleta matokeo chanya katika shule zote, kwani tayari kila Afisa Elimu Kata ameshatoa takwimu ya umbali kwa shule zake na umbali kuelekea Wilayani, na taarifa imetumwa kwa wafadhiri wa mradi wa tusome pamoja, kwa lengo la kutoa huduma ya mafuta kwa kila mwezi kulingana na bajeti ya mradi.

Nao maafisa Elimu Kata waliopata pikipiki hizo, wameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuwapatia pikipiki hizo, na kusema kuwa pikipiki hizo zitawasaidia sana kurahisisha utendaki wa kazi zao za elimu na kwamba hawatakuwa na kikwazo cha usafiri katika usimamizi na ufuatiliaji wa maendeleo ya Elimu katika shule zao.

Zoezi hilo limekuja baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Newala kupitia Idara ya Elimu kupokea jumla ya pikipiki 22 zilizofadhiriwa na mradi wa Tusome Pamoja ambao unafadhiri Mikoa saba hapa nchini ukiwemo Mkoa wa Mtwara.

Mkuuwa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangososngo akikabidhi pikipiki kwa mmoja kati ya Maafisa Elimu Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala tarehe 13/09/2018 Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Baadhi ya pikipiki kati ya 22 aina ya HONDA zilizofadhiriwa na mradi wa Tusome Pamoja kabla ya kukabidhiwa kwa Maafisa Elimu Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa