• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

DC Newala aendesha harambee ya ujenzi wa madarasa

Posted on: January 11th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Newala, Mhe. Aziza Mangosongo ameendesha harambee ya ujenzi wa madarasa mawili katika shule ya msingi Mtunguru B iliyopo kijiji cha Mtunguru, kata ya Mtunguru, Wilaya ya Newala.

DC Newala akihamasisha wananchi wakati wa zoezi la harambee, Alhamisi 10/01/2019 kijiji cha Mtunguru

Harambee hiyo ilifanyika siku ya Alhamisi, tarehe 10 Januari 2018 ambapo ilihudhuriwa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Newala, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Ndg. Mussa Chimae, wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Wilaya ya Newala, Wahe. Madiwani, viongozi na wananchi wa kijiji cha Mtunguru.

Aidha harambee hiyo imefanikisha kupatikana kwa fedha taslimu pamoja na ahadi ya fedha na vifaa vya ujenzi ambapo vyote vina jumla ya shilingi milioni kumi laki tisa elfu tisini na tisa na mia mbili.

Harambee hiyo imekuja baada ya wananchi wa kijiji cha Mtunguru kuonyesha nia ya kuwa na shule ya msingi katika kijiji chao ambapo mpaka sasa shule hiyo ina madarasa matatu, ofisi za walimu mbili na matundu ya vyoo matano vilivyojengwa kwa nguvu ya wananchi ambao walichangia kupitia zao la korosho ambapo kila mkulima alikatwa shilingi therathini kutoka katika kila kilo moja ya korosho, michangi ya shilingi elfu mbili kwa kila kaya na fedha kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Newala shilingi milioni kumi na tano na shilingi milioni moja na nusu kutoka katika mfuko wa jimbo.

Majengo ya madarasa na ofisi yanayotumika katika Shule ya msingi Mtunguru B kwa sasa

Shule hiyo ilifunguliwa rasmi mwaka 2016 ambapo mpaka sasa ina jumla ya wanafunzi 170.

Mhe.Mangosongo amewapongeza wananchi wa kijiji cha Mtunguru kwa kuona umuhimu wa elimu na alisisitiza wazazi kuhakikisha wanafunzi wanaripoti shule katika kipindi hiki ambacho shule zimefunguliwa na kuacha visingizio vya kutokuwa na fedha za kuwanunulia mahitaji watoto wao kwa kuwa Serikali imeshalipa shilingi bilioni ishirini na mbili kwa wakulima wa korosho wa Wilaya ya Newala na waliobaki wanaendelea kulipwa.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • MKUTANO MAALUM WA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI

    June 21, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa